JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

FIKRA YA HEKIMA

LAAC imechelewa kugundua
madudu hazina, halmashauri

Ijumaa iliyopita, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), ilitangaza kugundua mtandao wa wizi wa mabilioni ya shilingi za umma. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Rajab Mohamed Mbarouk, alisema mtandao huo unahusisha ofisi za Hazina na halmashauri mbalimbali hapa nchini.

BARUA ZA WASOMAJi

Bukoba kulikoni?

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meya, Balozi Kagasheki tuambieni kulikoni Bukoba? Tuambieni wakweli ni wapi kati ya madiwani waliofukuzwa, meya na madiwani waliobaki. Tuambieni tatizo ni nini hasa? Kimefichika nini hasa?

KAULI ZA WASOMAJI

Pongezi wana JAMHURI

Nawapongeza wafanyakazi wa Gazeti Jamhuri kwa kuanika wazi majina ya wauza unga katika toleo lililopita. Lakini kwanini serikali yetu isiwatie kitanzini kama huko China? Pia si hao tu, mafisadi nao watunguliwe risasi wazi wazi iwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya uovu huo.

 

Justus Julius Mwombeki, Bukoba

0753 191 029

Ponda naye anatafuta huruma ya waumini?

Mtakumbuka kuwa Agosti 10, mwaka huu, siku ya Idd Pili, iliisha vibaya kwa Katibu wa Jumuia na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda. Siku hiyo katika simu yangu uliingia ujumbe mmoja kutoka kwa watu zaidi 25. Ujumbe huo ulisomeka hivi ‘Sheikh Issa

Ponda amepigwa risasi Morogoro, wataarifu waumini wengine kumuombea na kukemea mashambulizi ya silaha dhidi yake’.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Tujifunze kusikiliza hoja za wengine

“Hatuna budi, hasa katika majadiliano na mazungumzo yanayohusu jumuiya, tujifunze kusikiliza hoja zilizotolewa na wenzetu, na kuzijibu kwa kuzikubali au kuzikataa, bila kujali kama aliyezitoa ni rafiki au si rafiki.”


Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Kwanza wa Tanganyika na baadaye Tanzania.

Dk. Mwakyembe sibipu, nakupigia mheshimiwa

Halo! Ni matumaini yangu kuwa uko hewani na unanisikia mheshimiwa. Nakuomba univumilie nimejiunga na mtandao wa Jamhuri kwa kuwa Voda, Tigo, Airtel na Zantel wameniambia salio langu halitoshi kuniwezesha niwe hewani kwa muda niutakao.