Category: Siasa
NUKUU ZA WIKI
Julius Nyerere: Mahitaji ya wananchi yalindwe
“Lazima tuendelee kuhakikisha kwamba mahitaji ya msingi ya watu wote yanapatikana na yanalindwa. Lengo letu lazima liendelee kuwa kuinua hali ya maisha ya kila mtu, na kila mtu aweze kupata huduma za msingi za elimu na matibabu.”
Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Hoja ni kutii sheria, si kufuta kauli
Hivi karibuni niliandika makala nikizungumzia kauli za wanasiasa na athari zake kwa umma. Nilizungumza kuhusu kauli zinazochochea vurugu, migongano na kuleta chuki na uvunjifu wa amani.
Mandela alifunguliwa milango ya gereza, akagoma kutoka
Ikiwa Mungu atapenda, maana hadi tunachapisha makala haya, Mzee wetu, mwana wa kweli wa Afrika, Nelson Rolihlahla Mandela maarufu kama Madiba, wa Afrika ya Kusini, Alhamisi wiki hii atatimizi miaka 95 ya kuzaliwa. Mandela anaumwa akisumbuliwa na ugonjwa wa maambukizi ya mapafu na amelazwa katika hospitali moja jijini Pretoria, nchini humo.
Vidonda vya tumbo na hatari zake (4)
Katika sehemu ya tatu ya makala haya, Dk. Khamis Zephania alieleza maana na sababu za fumbatio, vidonda vya umio na jinsi vidonda vya tumbo vinavyotokea. Sasa endelea kumfuatilia katika sehemu hii ya nne…
Ndoto ya pensheni kwa wazee wote kutimia (4)
Sehemu ya tatu ya mfululizo wa makala haya ilihoji kama kipo chama chochote cha wazee kushughulikia kilio chao, kuwasemea na wakasikika kama Umoja wa Vijana au Umoja wa Wanawake (UWT), au Umoja wa Wafanyakazi (TUCTA), au Umoja wa Wazazi (TAPA)? Mwandishi aliuliza, kwanini hali namna hiyo itokee kwa wazee? Mbona wapo wazee wasomi wengi tu wenye uwezo mkubwa wa kuongoza? Endelea.