JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

MKATA MITAA

WAWATA St. Joseph na bei za vyakula za ‘kitalii’

Kwa kawaida watu wanyonge wamezitambua nyumba za ibada kama sehemu ya ukombozi! Haishangazi kuwaona kina mama, kina baba, watoto, wazee na watu wasiojiweza wakikimbilia makanisani na misikitini kunapotokea vurugu.

FASIHI FASAHA

Mandela  ataenziwa au atakumbukwa?

Ni muda wa wiki tatu sasa, dunia imepata mzizimo na simanzi kutokana na kifo cha mtoto wa Afrika, shujaa, mpenda haki na usawa na kipenzi cha dunia, mtoto huyo ni Nelson Mandela. “Madiba.”

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

 

Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (11)

 

Katika sehemu ya kumi, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alisema kwa hiyo Waziri Mkuu alipomwambia Rais kwamba hoja ya Serikali Tatu ikijadiliwa Bungeni yeye mwenyewe atakuwa na utatizi wa uamuzi, alikuwa anajisemea kweli yake. Alikuwa katika hali hii ya “dilemma”. Baadaye, kama tunavyojua, alipoambiwa kuwa asipokubaliana na wenzake ataachwa katika mataa, aliamua kusarenda na wote wakaunga mkono hoja ya Utanganyika.

Ifuatayo ni sehemu ya kitabu cha Mwalimu Nyerere alichokiandika mwaka 1994 cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Endelea…

 

Hawa si watu wajinga, na wala  si wapumbavu; wanajua wafanyalo. Wamefanya uamuzi huu wakijua matokeo yake. Kwa hawa sasa, makosa ya “Wazanzibari” yawe ya kuvunja Katiba au ya aina nyingine, kwao sasa ni faraja; ni hoja ya kudai Utanganyika. Hawa hawawezi tena kutaka makosa hayo yazungumzwe na yasahihishwe; maana yakisahihishwa kama lilivyosahihishwa lile la OIC msingi wake wa hoja yao utabomoka.

Viongozi waige uzalendo wa Rais Jakaya Kikwete

 

Tumeambiwa kwamba Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) limesitisha mashindano ya Miss Utalii baada ya kuona uendeshaji wa mashindano hayo umekosa uzalendo na hauzingatii utamaduni wa Tanzania.

JAMHURI YA WAUNGWANA

Ujasiri huu wa ‘Wasukuma’ utufumbue macho Watanzania

Diwani wa Kisesa, Clement Mabina, ameuawa. Waliomuua ni wananchi, pengine wakiwamo wapigakura wake. Tumeziona picha zikimwonesha Mabina akiwa amepasuliwa kichwa na mwili wake ukiwa ndani ya dimbwi la damu na kando yake kukiwa na mawe makubwa. Waliomuua walifanya hivyo kana kwamba wanamuua mnyama hatari aliyeingia kwenye himaya ya binadamu! Ni jambo la kusikitisha.

FIKRA YA HEKIMA

 

Wabunge hawa hawatufai

 

Nianze kwa kuwapa pole mawaziri Shamshi Vuai Nahodha (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa), Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi) na Dk. Mathayo David Mathayo (Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi), waliopitiwa na rungu la Rais Jakaya Kikwete la kuvuliwa nyadhifa hizo, wiki iliyopita. Huo ndiyo uwajibikaji wa kisiasa.