Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amemtangaza kocha Emmanuel Amunike kutoka Nigeria kuwa kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars”.

Kocha huyo amefikia mwafaka na TFF ya kusaini kandarasi ya miaka miwili kuinoa Taifa Stars inayodhaminiwa na bia ya Serengeti.

Amunike aliwahi kutamba na kikosi cha Nigeria akicheza kama winga wa kushoto na pia alifanikiwa kuifundisha timu ya taifa hilo mwaka 1993 mpaka 2001.

Mchezaji huyo mstaafu alikiongoza kikosi cha timu ya taifa ya Nigeria katika mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 1994 kilichowafunga Bulgaria mabao 3-0 katika hatua ya makundi na pia kupoteza dhidi ya Italy kwa mabao 2-1 kwenye 16 bora.

Aidha Amunike anakumbukwa kwa kuisaidia Nigeria kutwaa taji la Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1994 huko Tunisia na baada ya mashindano hayo aliweza kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa Afrika.

By Jamhuri