NUKUU ZA WIKI

Mwalimu Nyerere: Vyama vijihadhari kutumiwa

“Shughuli za demokrasia lazima ziwe kazi ya kudumu katika chama cha kidemokrasia na katika taifa la kidemokrasia, vinginevyo chama hicho wakati wote kitakuwa katika hatari ya kutumiwa na wakorofi wachache tu.”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Obama: Sisi ndiyo mabadiliko tunayotafuta

“Mabadiliko hayawezi kuja kama tunasubiri watu wengine au wakati mwingine. Sisi ndiyo watu ambao tumekuwa tukisubiriwa kwa ajili hiyo. Sisi ndiyo mabadiliko tunayotafuta.”

Haya ni maneno ya Rais wa sasa wa Marekani, Barack Hussein Obama. Ni rais wa 44 wa taifa hilo.

 

Jacob Zuma: Wananchi wakiniagiza nitatekeleza

“Watu wengi katika nchi hii [Afrika Kusini] hawajaona kosa lolote juu yangu… Kama wengi wakisema, ‘Zuma, fanya hiki,’ nitakifanya.”

Hii ni kauli ya Rais wa Afrika Kusini, Jacob Gedleyihlekisa Zuma.

 

George Bush: Uongozi ni wajibu, heshima

“Kwangu uongozi una maana ya wajibu, heshima, nchi. Una maana ya tabia, na una maana ya kusikiliza mara kwa mara.”

Kauli hii ni ya Rais mstaafu wa Marekani, George Walker Bush. Ni rais wa 43 wa nchi hiyo.