“Wananchi wanapoonyesha makosa ya uamuzi wa kipumbavu wanatumia haki yao ya uraia. Wanaponung’unika kwa uamuzi ambao si wa kipumbavu wanaweza wakaelekezwa mpaka wakaelewa kwanini uamuzi ule ulifanyika, na faida zake ni nini.”

Nukuu hii ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyochukuliwa katika ukurasa wa 128-129 katika kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu Nyerere aliyezaliwa mwaka 1922. Alifariki dunia Oktoba 14, 1999.

 

Mandela – Uongozi

“Msinihukumu kwa mafanikio yangu, mnihukumu kwa kuangalia ni mara ngapi nilianguka na kuinuka tena.”

Nukuu hii ilitolewa na Rais wa kwanza wa Afrika Kusini Nelson Mandela, akiwahamasisha kutokata tamaa na kutimiza wajibu wao.

By Jamhuri