Latest Posts
VITA DHIDI YA UJANGILI Waraka muhimu wa Mch. Matwiga …1
Ndugu Watanzania wenzangu na Wizara ya Maliasili na Utalii, kwanza naomba kusema jambo moja kama Mtumishi wa Mungu, ambaye nimeitwa naye kwa maslahi ya mbingu, ili kuijenga jamii na umma kimaadili. Nitasimama siku zote katika “kweli” na hiki ndicho “kiapo changu” ee Mungu tusaidie.
Wanaoiponda UDA wamekosa uzalendo
Tumetafakari kwa kina juu ya taarifa zinazolaumu “Serikali kubariki ufisadi wa UDA.” Lawama hizo hutolewa na Watanzania wachache sana wanaopinga Kampuni ya wazawa ya Simon Group kuuziwa hisa za UDA.
Hoja za msingi malalamiko hayo ni kwamba Simon Group haikufuata taratibu na sheria, na pia kwamba haikuzingatia thamani halisi ya shirika hilo. Tunachofahamu sisi kwa sasa ni kwamba uuzwaji huo uko sahihi na hakuna kinachoweza kubadilika, kwani taratibu na sheria zote zilizingatiwa kikamilifu wakati wa uuzaji wa hisa za UDA kwa Simon Group.
Wamiliki mabasi wana wajibu wa kupunguza ajali
Tatizo la ajali za barabarani limekuwa ni moja ya changamoto kubwa sana katika sekta ya usafiri wa barabara hapa nchini. Katika kipindi cha mwanzo wa mwezi Septemba, 2014 kumetokea ajali za barabarni kubwa zaidi ya mbili katika mikoa ya Mara na Tabora, ambako watu zaidi ya 40 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa.
Ninachokumbuka kuhusu mradi wa maji Ziwa Victoria
Katika dunia kuna mambo yakitokea unajiuliza kwa nini yametokea. Unajiuliza ni hivi hivi au kuna msukumo, ila yote kwa yote nimejiwekea utaratibu wa kusimamia ukweli. Mara zote naamini ukweli unamweka mwanadamu huru, na hapa leo kama nifanyavyo siku zote nitajaribu kueleza ukweli ninaoufahamu.
Ukweli kuhusu elimu ya Lembeli
Mwalimu Julius Nyerere, ambaye Mheshimiwa James Lembeli amewahi kujifananisha naye, aliwahi kusema kuwa ikitokea mtu wa kawaida akampiga mkewe hadharani, hii haiwezi kuwashughulisha watu na wala haiwezi kuwa habari. Lakini ikatokea yeye (Mwalimu) akafanya hivyo, basi hiyo itakuwa habari kubwa mno.
Mwalimu Nyerere na mgombea binafsi
Mei Mosi, 1995 Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, akiwa mgeni rasmi kwenye Sherehe za Mei Mosi mjini Mbeya, alizungumza mambo mengi yaliyolihusu Taifa. Miongoni mwa mambo hayo ni haki ya kuwapo mgombea binafsi. Rasimu ya Katiba Mpya (ya Jaji Warioba) ilizingatia jambo hili muhimu. Hata hivyo, Bunge Maalum la Katiba (katika Rasimu ya Samuel Sitta) limeminya mno haki ya kuwapo mgombea binafsi. Ilivyo ni kama haki hiyo haipo kwani imewekewa vizingiti vizito mno. Soma maneno haya ya Mwalimu Nyerere.