JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Navumilia kuwa Mtanzania

Tanzania ni nchi yangu ninayoipenda kwa moyo wote, ni kisiwa cha amani, upendo na utulivu, ni nchi yenye watu wakarimu na wenye upendo na mahaba yasiyopimika. Watanzania wanaishi kwa kupendana kuthaminiana na kuheshimiana bila kujali matatizo au changamoto zinazowakabili, kila mmoja akimuita mwenzake ndugu.

Sasa ianzishwe Mahakama ya dawa za kulevya, ujangili

Vita dhidi ya dawa za kulevya inahitaji msukumo, mbinu na sheria mpya. Hii si vita ya Polisi, Usalama wa Taifa wala Serikali pekee. Wala vita hii hatuwezi kuishinda kwa kubaki tukioneana haya au tukiogopana.

Kwa wiki kadhaa, vyombo vya habari, tukiwamo sisi JAMHURI, tumeamua kwa dhati kabisa kuishiriki vita hii. Tumefanya hivyo kwa kutambua madhara makubwa yanayosababishwa na matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana wetu.

JAMHURI YA WAUNGWANA

Kuanzia kitongoji hadi
Ikulu wote wanalalamika

Siku kadhaa zilizopita nilikutana na mwanahabari mwenzangu, Khalfan Said. Aliniuliza swali hili; “Huu uamuzi wa Rwanda na Uganda kususa bandari zetu utakuwa na athari gani kwa uchumi wetu.” Khalfan aliniuliza swali hili akitambua kuwa mimi si mchumi. Hilo analitambua vema. Mara moja nikatambua kuwa tunao kina Khalfan wengi wanaotaabishwa na jambo hili, kiasi kwamba wapo radhi kumuuliza yeyote wanayemwona hata kama wanajua si mtaalamu wa masuala ya uchumi.

Meya, mbunge Ilemela bado kunachimbika

Mgogoro baina ya Meya wa Manispaa ya Ilemela, Mstahiki Henry Matata, na Mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia, unaendelea kufukuta na kujenga makundi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Hatujajipanga kuleta BRN katika elimu

Baada ya kuona kuwa wameboronga elimu na wameendelea kusemwa vibaya, sasa Waziri wa Elimu na wasaidizi wake wamekuja na  jambo jipya kwa lengo la kujikosha. Wamekuja na mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now-BRN).

Mchapishaji vitabu adaiwa kumdhulumu Halimoja

 

Mmiliki wa kampuni ya Educational Books Publishers ya jijini Dar es Salaam, anadaiwa kumdhulumu mwandishi mahiri na mkongwe wa vitabu nchini, Mzee Yusuf Halimoja. Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kwamba mwaka 2010 mchapishaji huyo wa vitabu na Mzee Halimoja walikubaliana kwamba mwandishi huyo aandike vitabu vya kiada vya masomo ya uraia na historia vya darasa la saba.