HUU HAPA MSIMAMO WA CHADEMA KUHUSU UCHAGUZI JIMBO LA KINONDONI

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeeleza kuwa, bado msimamo wake na vyama vingine vinne vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kuhusu kutokushiriki uchaguzi wa marudio katika jimbo la Kinondoni na sehemu nyingine na kwamba msimamo wao uko pale pale na hakuna maamuzi mengine yaliyotolewa hadi sasa.

Ikumbukwe katika Jimbo la Kinondoni uchaguzi utarudiwa kutokana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Dkt. Mtulia kujivua uanachama na kuahamia CCM, lakini hata hivy Mtulia amechaguliwa tena na CCM kugombea tena Katika Jimbo hilo la Kinondoni.