JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mapapa wa ‘unga’ watajwa

*Kinondoni, Magomeni, Mbezi, Tanga watia fora

*Wamo Wakenya, Wanigeria, waimba taarab Dar

*Wengine wapata dhamana kimizengwe, watoroka

Vita dhidi ya wauzaji na wasafirishaji dawa za kulevya inazidi kupamba moto, na sasa JAMHURI imepata orodha ya watu wengine 245 wanaotajwa kuwa ndiyo ‘mapapa’ wa biashara hiyo haramu hapa nchini.

Yah: Tunashindwaje kukabili vifo vya kujitakia?

Nataka niwe mtu wa tatu kupigana na utaratibu wa maisha ya Mtanzania kuwekewa mazingira ya kifo ambayo hakustahili, mazingira haya yanatayarishwa bila mtayarishaji na anayetayarishiwa kujua kuwa anaandaliwa mazingira ya kifo.

KONA YA AFYA

Vidonda vya tumbo na hatari zake (9)

Katika sehemu ya nane ya makala haya, Dk. Khamis Zephania alizungumzia pamoja na mambo mengine, madhara ya kazi za usiku, makundi ya damu na uhusiano wa vidonda vya tumbo. Sasa endelea na sehemu hii ya tisa…

KAULI ZA WASOMAJI

Pongezi wana JAMHURI

Nawapongeza wafanyakazi wa Gazeti Jamhuri kwa kuanika wazi majina ya wauza unga katika toleo lililopita. Lakini kwanini serikali yetu isiwatie kitanzini kama huko China? Pia si hao tu, mafisadi nao watunguliwe risasi wazi wazi iwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya uovu huo.

 

Justus Julius Mwombeki, Bukoba

0753 191 029

Bukoba nani anasema ukweli?

Nchi hii kila kukicha inaacha maswali mengi. Mwanzo niliamua kunyamaza, lakini leo naona ni bora nihoji. Nahoji kutokana na taarifa zinazosambaa na kuzua mgogoro mkubwa ajabu katika mji wa Bukoba. Hapa inadaiwa kuna mapapa wawili – Mbunge Balozi Khamis Kagasheki na Meya Anatory Amani.

Wajasiriamali na mfupa wa huduma kwa wateja

Siku moja nilikuwa mjini Mafinga wilayani Mufindi katika Mkoa wa Iringa. Nikiwa hapo niliingia kwenye duka moja la vifaa vya ujenzi nikiwa na lengo la kununua vifaa kadhaa vyenye thamani ya takribani shilingi laki tatu.