Latest Posts
Mapapa wa ‘unga’ watajwa
*Kinondoni, Magomeni, Mbezi, Tanga watia fora
*Wamo Wakenya, Wanigeria, waimba taarab Dar
*Wengine wapata dhamana kimizengwe, watoroka
Vita dhidi ya wauzaji na wasafirishaji dawa za kulevya inazidi kupamba moto, na sasa JAMHURI imepata orodha ya watu wengine 245 wanaotajwa kuwa ndiyo ‘mapapa’ wa biashara hiyo haramu hapa nchini.
Yah: Tunashindwaje kukabili vifo vya kujitakia?
Nataka niwe mtu wa tatu kupigana na utaratibu wa maisha ya Mtanzania kuwekewa mazingira ya kifo ambayo hakustahili, mazingira haya yanatayarishwa bila mtayarishaji na anayetayarishiwa kujua kuwa anaandaliwa mazingira ya kifo.
KONA YA AFYA
Vidonda vya tumbo na hatari zake (9)
Katika sehemu ya nane ya makala haya, Dk. Khamis Zephania alizungumzia pamoja na mambo mengine, madhara ya kazi za usiku, makundi ya damu na uhusiano wa vidonda vya tumbo. Sasa endelea na sehemu hii ya tisa…
KAULI ZA WASOMAJI
Pongezi wana JAMHURI
Nawapongeza wafanyakazi wa Gazeti Jamhuri kwa kuanika wazi majina ya wauza unga katika toleo lililopita. Lakini kwanini serikali yetu isiwatie kitanzini kama huko China? Pia si hao tu, mafisadi nao watunguliwe risasi wazi wazi iwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya uovu huo.
Justus Julius Mwombeki, Bukoba
0753 191 029
Bukoba nani anasema ukweli?
Nchi hii kila kukicha inaacha maswali mengi. Mwanzo niliamua kunyamaza, lakini leo naona ni bora nihoji. Nahoji kutokana na taarifa zinazosambaa na kuzua mgogoro mkubwa ajabu katika mji wa Bukoba. Hapa inadaiwa kuna mapapa wawili – Mbunge Balozi Khamis Kagasheki na Meya Anatory Amani.
Wajasiriamali na mfupa wa huduma kwa wateja
Siku moja nilikuwa mjini Mafinga wilayani Mufindi katika Mkoa wa Iringa. Nikiwa hapo niliingia kwenye duka moja la vifaa vya ujenzi nikiwa na lengo la kununua vifaa kadhaa vyenye thamani ya takribani shilingi laki tatu.