JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Siri ya mafanikio yangu kiuchumi – 2

Wiki iliyopita nilieleza namna changamoto za kiuchumi zinavyowahenyesha wafanyakazi. Pia nilianza kueleza mchapo unaonihusu wa namna nilivyopambana kujikwamua kiuchumi nikiwa nimeajiriwa kwa kazi ya ualimu. Leo nitahitimisha kwa kubainisha mbinu kadhaa ili kumudu mchakamchaka wa maisha ya kiuchumi. Endelea…

Museveni: Waafrika hatujui kuomba

“Tatizo letu sisi Waafrika hatujui kuomba, na hata tunapopata fursa ya kuomba hatuombi kwa akili. Nilipokwenda kwa Gaddafi [wakati napigana vita ya kumuondoa Idi Amin) aliniuliza ‘Nikupe pesa?’ Nikasema hapana. Akasema ‘Nikupe sare za askari?’ Nikamwambia hapana. Akasema ‘Unataka nini sasa kwangu?’ Nikamwambia bunduki na risasi.”

Yanga, Simba ‘fowadi’ mbovu

Ikiwakilishwa na timu nne za Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club, Dar es Salaam Young Africans (Yanga), Azam FC zote za jijini na Mafunzo kutoka Zenji katika hatua za awali za michuano ya Kombe la Kagame, Tanzania ilipata fedheha kubwa katika mechi zilizochezwa siku ya kwanza na ya pili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mke wa Msekwa, wenzake wanavyotafuna nchi

*Kikao cha siku moja walipata Sh milioni 7

*Mjumbe mmoja asaini posho mara mbili

*Mkewe Mudhihir ambaye si mjumbe alipwa

 

Ufisadi unazidi kuwaandamana viongozi wa CCM. Safari hii, Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Abdallah, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo, wanatuhumiwa kujilipa mamilioni ya shilingi. Ulaji huo umefichuliwa na Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Rose Kamili, katika hotuba yake ya makaridio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha wa 2012/2013

 

BODI ZA MAZAO YA BIASHARA NA MAENDELEO YA KILIMO

Mheshimiwa Spika, kilimo cha mazao ya biashara hapa nchini kwa sasa kina changamoto nyingi. Changamoto hizo ni pamoja kukosa soko na bei za uhakika za mazao hayo.

Yah: Nahisi sasa kuwa ni mganga wa kienyeji

Tangu zamani dhana kwamba mtu mzee ndiye mchawi katika jamii, imejengeka sana miongoni mwa walio wengi wenye upeo mdogo wa kufikiri na kuiaminisha jamii yenye maadili mema kuwa na imani potofu kwa sisi wazee.

Vita kubwa TANESCO

*Wabunge wajiandaa kukwamisha tena bajeti ya Wizara ya Nishati, wahoji zabuni ya mafuta BP

 *Wajiandaa kuwang’oa Waziri Profesa Muhongo, Katibu Mkuu Maswi Ijumaa ya wiki hii

 *Katibu Mkuu aanika ukweli, asema Wizara yake haikufanya manunuzi waliohusika ni RITA, Zitto anena

[caption id="attachment_219" align="alignleft" width="243"]Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Peter MuhogoWaziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo[/caption]Kuna kila dalili kuwa imeibuka vita ya wazi kati ya Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), huku Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco aliyesimamishwa kazi, William Mhando, akipigiwa debe la wazi na wabunge.

Taarifa zilizopatikana kwenye ofisi za Bunge zinasema kuwa Kamati ya Nishati na Madini inajipanga kukwamisha bajeti ya wizara hiyo kama Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco aliyesimamishwa kazi, Injinia Mhando, hatarejeshwa kazini huku wizara ikisisitiza kuwa amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi wala hajafukuzwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, naye ana msimamo kuwa Mhando ameonewa na wizara inaweza kujiokoa kwa kumrejesha ofisini kisha ufanywe uchunguzi maalumu utakaoendeshwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).