Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwaapisha Mawaziri Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Angellah Jasmine Kairuki kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Dkt. Stergomena Lawrence Tax kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Oktoba, 2022.
Waziri wa TAMISEMI Angellah Jasmine Kairuki, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Innocent Lugha Bashungwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Stergomena Lawrence Tax wakiapa Kiapo cha Maadili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Oktoba, 2022.

By Jamhuri