Ajali ya barabarani Uganda yauwa 23, kujeruhi 25

Watu 23 wamefariki dunia na wengine 25 wamejeruhiwa kwa ajali mbaya basi iliyotokea wilaya ya Kiryandongo nchini Uganda.
Polisi wamesema basi linalomilikiwa na kampuni ya Gaagaa bus liligonga trekta kwa nyuma na baada ya hapo, kupoteza muelekeo na kusababisha kugongana uso kwa uso na gari la mizigo lililokuwa limebeba kreti za bia, ambalo lilikuwa linatokea Kampala.
“Watu 19 walipoteza maisha papo hapo wakiwemo madereva. Watu wengine 25 walikimbizwa hospitali kwa usafiri wa ndege ya Serikari ya Uganda na kulazwa katika hospitali ya Kiryandongo.

#Poleni sana ndugu zetu Waganda