Category: Siasa
Wataalamu: Mtoto mpotevu Dar ana tatizo la kisaikolojia
Wanataaluma nchini wamesema kwamba wamefuatilia habari za kupotea na kupatikana kwa mtoto Happy Rioba (9), na kwa haraka wamegundua kwamba binti huyo ana tatizo la saikolojia tofauti na wengi wanaohusisha ushirikina.
Happy, anayeishi na mama yake, Sarah Zefania huko Mkuranga mkoani Pwani, aliripotiwa na vyombo vya habari kupotea na kupatikana zaidi ya mara moja, tukio lililovuta hisia za watu wengi.
Kwa mtego huu wa UKAWA hautamnasa Rais Kikwete
Tukio la hivi karibuni ambapo wajumbe wanaounda kundi la Umoja wa Katiba wa Wananchi (UKAWA) kuamua kuyakana makubaliano yaliyofikiwa baina yao na Rais Kikwete kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), haliwezi kupita bila kuhojiwa.
Mbowe moto
.Adai moto aliowasha hauzimiki mpaka kieleweke 2015
.Asema anaumizwa kuteketea mamilioni Bunge la Katiba
.Atamba ipo siku polisi watazitambua haki za Watanzania
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema anashangazwa na vigogo wa Jeshi la Polisi kufanya hila za kumkabili, ilhali wanaona namna Watanzania walivyodhulumiwa haki yao kupitia Bunge Maalum la Katiba.
Tanzania yaonywa kuhusu Al-Shabaab
POLISI wa Uganda wameitaka Tanzania kuwa makini na kundi la ugaidi la Al-Shabaab kutoka Somalia, baada ya jeshi hilo kuwakamata watu wanaotuhumiwa kufanya vitendo vya kigaidi.
Tukio hilo limekuja siku chache baada ya Kenya kujihami kwa Polisi wao kumuua kwa risasi mtuhumiwa wa ugaidi katika maeneo ya Bondeni mjini Mombasa.
Ni Polisi tena
Siku chache baada ya Jeshi la Polisi nchini kukutana na wadau wa habari na kuwataka waripoti habari zinazozingatia amani na usalama wa nchi pamoja na kuwafanya raia wawe na imani na jeshi hilo, baadhi ya polisi wamekuwa vinara wa kuendeleza vitendo vya udhalilishaji na unyanyasaji wa raia, huku mara kwa mara wakitumia nguvu kubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Tanzania yaongoza kuvutia uwekezaji
Imeelezwa kuwa Tanzania imeshika nafasi ya kwanza katika nchi zinazovutia uwekezaji katika nchi za Afrika Mashariki. Kadhalika Tanzania inashika nafasi ya tisa barani Afrika.