Category: Siasa
Kitanzi cha JK
Wizara ya Maliasili yatajwa kuwa mtego kwa Kikwete
Pinda, Mwamunyange, Mwema watakiwa kupima uzito
Rais Jakaya Kikwete, akiwa anatarajiwa kulisuka upya Baraza la Mawaziri, kuna kila dalili kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sasa ndio imebaki kuwa kitanzi kinachotishia uhai wa Serikali yake.
Siri ya Mandela
*Alisahau viatu vyake vya kijeshi Tanzania, akafungwa
*Mufti Simba, Askofu Kilaini, Ruwa’ichi watoa tamko
*Profesa Baregu, Wangwe, Safari, Kiwanuka wanena
Kifo cha Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela “Madiba”, kimefichua siri nzito kuhusu harakati zake za ukombozi wa taifa hilo kutoka katika makucha ya serikali ya kibaguzi ya Wazungu.
M23 yawafika mazito
*UN waanza kutumia ndege zisizo na rubani kusaka masalia
*Zinatambua aliko mwenye bunduki, zilitumika Afghanistan
Baada ya Brigade Maalum ya Umoja wa Mataifa ikiongozwa na Jenerali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuwasambaratisha waasi wa M23 nchini DRC, Brigade hiyo imeanza kutumia ndege zisizokuwa na marubani (drones) kufanya ulinzi katika mji wa Goma, hali inayozidi kuwafukizia moshi waasi hao.
Jahazi Asilia: CCM, CUF wanahofu vivuli vyao
Chama cha Jahazi Asilia kimesema mtindo unaotumiwa na vyama vya CCM na CUF kubeba wanachama kwenda na kurudi kwenye mikutano ya hadhara hauvikisaidii vyama hivyo kujitambua na kupima kisiasa kama vinakubalika au la.
M23 walia njaa
Waona giza nene mbele yao, Uganda yaonya vita inanukia
DRC yazidisha mashaka kwa Uganda, Watanzania waonya
Hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kukataa kusaini mkataba wa amani na kundi la waasi la M23, imepeleka kilio kwa kundi hilo, na sasa wanalia njaa uhamishoni nchini Uganda.
Wastaafu wahoji hati ya Muungano Pemba, Unguja
Wastaafu wa kada mbalimbali serikalini wameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) chini ya Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, kuonesha hati ya Mungano wa Unguja na Pemba iwapo visiwa hivyo viliungana kisheria na mkataba kutambuliwa na Umoja wa Mataifa.