Category: Maoni ya Mhariri
Kikwete anastahili pongezi
Wiki iliyopita ilikuwa na matukio makuu mawili. Tukio la kwanza ni Alhamisi, ambapo Rais Jakaya Kikwete alihutubia Bunge. Alisema bayana kuwa alikwenda bungeni kuzungumza suala moja tu la msingi, ingawa alichomekea mengine. Suala hili ni mustakabali wa Tanzania ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Operesheni Tokomeza ilistahili, waliofanya uhuni waadhibiwe
Wiki iliyopita Bunge limetoa maelekezo kwa Kamati ya Maliasili na Utalii kuchunguzia utekelezaji na mwenendo wa Operesheni Tokomeza. Operesheni hii imeendeshwa kwa makusudi kudhibiti majangili waliokuwa wakiua tembo kwa kasi ya ajabu na kutishia uwepo wa tembo nchini. Wabunge wamelalamika kuwa askari walioendesha operesheni hii walikosa uaminifu.
Nishati na Madini ni Mfano wa kuigwa
Mwishoni mwa wiki iliyopita Wizara ya Nishati na Madini iilitoa taarifa ya utekelezaji wa kipindi cha miezi mitatu iliyopita chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BNR).
Hakimu huyu ashughulikiwe
Katika toleo la leo tumechapisha habari za kusikitisha juu ya matumizi mabaya ya madaraka katika Idara ya Mahakama Tanzania. Tumechapisha habari kuwa mtuhumiwa mwenye asili ya China alikamatwa Alhamisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akiwa na madini ya tanzanite yenye thamani karibu Sh milioni 200.
Mwalimu asienziwe kwa porojo
Miaka 14 imeshatimia tangu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alipofariki dunia katika Hospitali ya Mtakatifu Thomas jijini London, Uingereza, Oktoba 14, 1999.
Tuwe makini, mitandao ya uhalifu inaongezeka
Kwa muda sisi JAMHURI tumekuwa tukiandika habari zinazohusu wasafishaji na wauza mihadarati; na pia matapeli wa biashara ya madini waliokubuhu. Tulichobaini ni kwamba wahusika wakuu kwenye biashara, hii wanalindwa na baadhi ya viongozi wakubwa katika nchi yetu. Mitandao ya uhalifu katika Tanzania ni mipana na yenye nguvu kuanzia ngazi za chini hadi katika vyombo vya ulinzi na usalama.