Category: Maoni ya Mhariri
Profesa Kapuya achunguzwe
Wiki iliyopita Taifa limetikiswa na habari za waziri wa zamani wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Profesa Juma Kapuya, kutuhumiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka 16.
Kikwete anastahili pongezi
Wiki iliyopita ilikuwa na matukio makuu mawili. Tukio la kwanza ni Alhamisi, ambapo Rais Jakaya Kikwete alihutubia Bunge. Alisema bayana kuwa alikwenda bungeni kuzungumza suala moja tu la msingi, ingawa alichomekea mengine. Suala hili ni mustakabali wa Tanzania ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Operesheni Tokomeza ilistahili, waliofanya uhuni waadhibiwe
Wiki iliyopita Bunge limetoa maelekezo kwa Kamati ya Maliasili na Utalii kuchunguzia utekelezaji na mwenendo wa Operesheni Tokomeza. Operesheni hii imeendeshwa kwa makusudi kudhibiti majangili waliokuwa wakiua tembo kwa kasi ya ajabu na kutishia uwepo wa tembo nchini. Wabunge wamelalamika kuwa askari walioendesha operesheni hii walikosa uaminifu.
Nishati na Madini ni Mfano wa kuigwa
Mwishoni mwa wiki iliyopita Wizara ya Nishati na Madini iilitoa taarifa ya utekelezaji wa kipindi cha miezi mitatu iliyopita chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BNR).
Hakimu huyu ashughulikiwe
Katika toleo la leo tumechapisha habari za kusikitisha juu ya matumizi mabaya ya madaraka katika Idara ya Mahakama Tanzania. Tumechapisha habari kuwa mtuhumiwa mwenye asili ya China alikamatwa Alhamisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akiwa na madini ya tanzanite yenye thamani karibu Sh milioni 200.
Mwalimu asienziwe kwa porojo
Miaka 14 imeshatimia tangu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alipofariki dunia katika Hospitali ya Mtakatifu Thomas jijini London, Uingereza, Oktoba 14, 1999.