Category: Maoni ya Mhariri
Serikali isikilize kilio cha Waislamu
Septemba 23, mwaka huu Baraza la Wakuu wa Shule za Kiislamu Tanzania wamemwandikia barua Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa kupinga utaratibu mpya wa mitihani na upangaji madaraja kuhusu masomo ya dini ya Kiislamu, kompyuta, lugha za Kiarabu, Bible Knowledge na Kifaransa. Masomo haya sasa yamegeuzwa ya hiari.
CAG awahishe ukaguzi Bukoba
Katika toleo la leo tumechapisha habari za mgogoro unaoendelea kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba. Mgogoro huu ni mkubwa kwa kiwango ambacho wananchi, watendaji, viongozi, wafanyabiashara na hata wanasiasa wamefika mahala hawaaminiani. Kila kona ya Bukoba kuna mazungumzo kwenye makundi.
Sote tukiwa waoga nchi itayumba
Ni kosa kubwa kwa mtoto wa Kizanaki kumtamkia mtu aliyemzidi umri neno ‘mwongo’. Hawa ni tofauti na makabila mengine, mathalani Wajita. Wao mtoto ana uhuru na haki ya kumtamkia mzazi au mtu aliyemzidi umri neno ‘mwongo’. Wakati Mzanaki atapambana kumnasa vibao mtoto anayeamini kamtukana, mzazi wa Kijita atafanya juhudi za kupambana kwa hoja kumthibitishia mtoto yule kwamba yeye (mkubwa) si mwongo. Hizo ni tofauti za wazi kwa makabila hayo mawili.
Matakwa ya Rwanda yasiivunje EAC
Kwa muda wa mwezi mmoja sasa uhusiano baina ya Tanzania na Rwanda umezorota. Uhusiano huo umezorota baada ya matukio mawili. Tukio la kwanza ni ushauri Rais Jakaya Kikwete aliompa Rais Paul Kagame wa kuzungumza na waasi wa kundi la FDLR kwa nia ya kurejesha amani. La pili ni Tanzania kupeleka majeshi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kupambana na waasi wa M23.
Sasa ianzishwe Mahakama ya dawa za kulevya, ujangili
Vita dhidi ya dawa za kulevya inahitaji msukumo, mbinu na sheria mpya. Hii si vita ya Polisi, Usalama wa Taifa wala Serikali pekee. Wala vita hii hatuwezi kuishinda kwa kubaki tukioneana haya au tukiogopana.
Kwa wiki kadhaa, vyombo vya habari, tukiwamo sisi JAMHURI, tumeamua kwa dhati kabisa kuishiriki vita hii. Tumefanya hivyo kwa kutambua madhara makubwa yanayosababishwa na matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana wetu.
Kamati Kuu CCM ikomeshe mgogoro unaofukuta Bukoba
Wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanajipanga kukutana wiki hii kutafuta ufumbuzi wa mgogoro mkubwa unaoendelea kufukuta katika Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, mkoani Kagera. Imeshadhihirika wazi kuwa mgogoro huo ni baina ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini na Meya Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani.