JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Maoni ya Mhariri

Wakenya heshimuni matokeo ya uchaguzi

Uchaguzi Mkuu wa Kenya ulimalizika jana kwa utulivu na amani, licha ya kuwapo kwa dosari ndogondogo, ikilinganishwa na wa mwaka 2007. Watu wengi duniani wameshuhudia na kusikia jinsi wananchi walivyojitokeza kwa wingi, kutumia haki yao ya kikatiba na kidemokrasia kuchagua viongozi watakaowaongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Serikali imdhibiti mwekezaji huyu

Moja ya habari zilizobeba uzito wa juu katika gazeti hili ni ile inayomhusu raia wa Uswisi, Dk. George Hess, anayetuhumiwa kumiliki na kuuza ufukwe wa Amboni uliopo Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga kinyume cha sheria.

Tutaijutia amani tunayoichezea

Kwa muda wa mwezi sasa nchi yetu ipo katika migogoro isiyomithilika. Yamekuwapo matukio yanayotia shaka iwapo sisi wazazi tuna hakika na tunachostahili kuwapatia watoto wetu. Kule Mwanza na Geita yametokea mauaji yaliyotokana na mapigano kati ya Wakristo na Waislamu wakigombea kuchinja wanyama.

Tuondokane na bima za magari

Kwa wiki nzima sasa kuna mjadala unaoendelea hapa nchini juu ya mpango wa kurekebisha viwango vya malipo ya bima ifikapo Machi mosi. Mpango huu unalenga hasa bima kubwa (premiums). Wanalenga kuweka viwango vya kati ya asilimia 3.5 hadi 9 kwa kila gari. Hawakuzungumzia suala la bima ndogo (third part).

Upungufu wa dawa, wafadhili ni hatari

Shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi ya kuboresha utawala bora, uwazi na uwajibikaji katika sekta ya afya na Ukimwi, SIKIKA, wiki iliyopita limetoa taarifa yenye kushtua juu ya upatikanaji wa dawa na wagharimiaji.

Mtwara wapewe asilimia mbili

Kwa muda wa mwezi mzima wananchi wa Mkoa wa Mtwara wapo kwenye maandamano. Maandamano haya yanaelekea kulifikisha taifa katika uvunjifu wa amani. Wananchi wanatumia nguvu, na kuna uwezekanao Serikali nayo itafika mahala itaishiwa uvumilivu itaanza kutumia nguvu. Mungu apishe mbali.