Dk. Kawambwa mtuhumiwa Na 1
Wiki iliyopita tuliandika maoni tukichagiza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aanzishe mchakato wa kufukuzwa kazi katika Baraza la Mitihani Tanzania, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Joyce Ndalichako. Tulisema uamuzi wa Baraza la Mitihani (NECTA) kubadili mfumo wa kuchakata matokeo na kufanya wanafunzi wengi kushindwa hauvumiliki.