Dk. Kawambwa mtuhumiwa Na 1

Wiki iliyopita tuliandika maoni tukichagiza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aanzishe mchakato wa kufukuzwa kazi katika Baraza la Mitihani Tanzania, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Joyce Ndalichako. Tulisema uamuzi wa Baraza la Mitihani (NECTA)  kubadili mfumo wa kuchakata matokeo na kufanya wanafunzi wengi kushindwa hauvumiliki.

Read More

Pinda mfukuze kazi Ndalichako

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi, wiki iliyopita amelitangazia Bunge uamuzi mgumu wa Serikali. Ametangaza kuwa Serikali sasa imeamua kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa 2012. Katika mtihani huo wanafunzi asilimia 65.5 walipata daraja sifuri.

Read More

Tukatae udini, ukabila nchini

Nchi yetu inapitia wakati mgumu. Udini umetamalaki kila kona. Zanzibar wanasema yao. Kanda ya Ziwa ndiyo usiseme. Mgogoro wa kuchinja umeibua mapya. Tayari Wakristo wana bucha zao, na hata wasio na bucha wanakusanyana wananunua ng’ombe wanachinja na kuuziana nyama kienyeji.

Read More

Maskini Bunge letu!

Watanzania tumepata mshituko. Tumeshangazwa na mwenendo wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tumeshangazwa na jinsi siasa zilivyoanza kugeuzwa uadui. Tumeshangazwa na jinsi wabunge walivyoanza kupoteza heshima na kushindwa kujitambua.

Read More

Tuunge mkono mkakati wa TRA

Wiki iliyopita Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza mkakati mpya wa ukusanyaji mapato. Mkakati huu mpya ulitangazwa mbele ya Wahariri wa vyombo vya habari nchini siku ya Alhamisi. Mkutano huo ulimhusisha Mkurugenzi wa Elimu kwa Walipakodi, Richard Kayombo na Naibu Kamishna (Mapato ya Ndani), Jenerose Bateyunga.

Read More