NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Chama kisilazimishe watu kukichangia fedha

“Kwamwe chama [cha siasa] kisitoze kodi, au ushuru, au malipo ya nguvu-nguvu kwa mtu yeyote, awe mwanachama au si mwanachama. Michango yoyote ya fedha inayotolewa kwa ajili ya shughuli za chama lazima itokane na ridhaa ya mtoaji mwenyewe.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Read More

WACHONGA VINYAGO MWENGE:

Hazina ya sanaa, utalii, utamaduni isiyovuma

*Wapo wanaoongozwa na mawingu kuchonga mashetani

*Wamarekani wapendelea ‘mashetani’, Waingereza ‘wanyama’

*Baadhi watumia ‘calculator’ kuwasiliana na wateja Wazungu

*Walilia soko la uhakika, waishutumu Serikali kuwapa kisogo

Umewahi kuzuru kituo cha wachongaji na wauzaji vinyago cha Mwenge, jijini Dar es Salaam? Kama bado, basi fanya hima ufike ujionee hazina ya sanaa, utalii na utamaduni wa Kitanzania iliyotamalaki, ingawa haivumi.

Read More

KAULI ZA WASOMAJI

Stendi ya Nyegezi ni jehanamu

Stendi ya mabasi ya Nyegezi, Mwanza ni mithili ya jehanamu, utapeli na usumbufu vimekithiri. Kwanini stendi za Tanzania zimeachwa kuwa vituo vya uhalifu wa kila aina, huku polisi wapo? Uchunguzi zaidi ufanyike kusaidia wananchi.

Rwambali F, Mwanza

Read More