Mtu mmoja amekufa na wengine watano kujeruhiwa katika maandamano ya kiuchumi katika mji mkuu wa Tunisia, tunis. Maandamano hayo yameenea katika maeneo mengine kumi nchini humo.

Uchumi wa nchi hiyo umekua ukitetereka tangu mwaka 2011 wakati kiongozi wa kipindi hicho Zine El Abdine Ben Ali akiondolewa madarakani.

Kwa sasa fedha ya Tunisia imeshuka zaidi ikilinganishwa na Uero,

Miongoni mwa sababu ya maandamano hayo ni mfumko wa bei ambao umesababisha kuongezeka kwa kodi katika bidhaa zinaingizwa nchini kama magari na bidhaa nyingine.

Shirika la habari la Tunisia limesema kuwa Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji wanaopinga kupanda kwa bei katika bidhaa mbalimbali katika maeneo mbalimbali.

Watu wengine Zaidi ya mia tatu wameingia barabarani katika mji wa kati wa Sidi Bouzid, huku wakipinga juu ya ukosekani wa ajira na maendeleo hafifu katika maeneo yao .

Tunisia inategemea misaada kutoka nje kupanda na kuporomoka kwake kwa uchumi,Na hii yote ni matokeo ya mapinduzi ya 2011 na mashumbulio mawili makubwa mwaka 2015 ambapo bado athari yake ni kubwa katika sekta ya utalii nchini humo.

By Jamhuri