Nyerere: Miiko ya uongozi

“Siku hizi fedha ndio sifa kubwa ya mtu kuchaguliwa kuwa kiongozi. Miiko ya uongozi ambayo ni jambo la lazima katika kila nchi duniani, haipo tena hapa nchini.”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Dalai: Jiamini ujenge ulimwengu

“Wakati mtu akitambua nafasi ya kujiamini yeye mwenyewe anaweza kujenga ulimwengu ulio bora zaidi.”

Haya yalisemwa na kiongozi wa Watibeti wapigania uhuru wa Jimbo la Myanmar, Dalai Lama.

 

Newton: Siwezi kuhesabu ukichaa

“Naweza kuhesabu mwendo wa viumbe wa angani, lakini sio ukichaa wa watu.”

Ni maneno ya mtaalamu maarufu wa Fizikia na Hisabati duniani, Isaac Newton wa nchini Uingereza.

 

Jackson: Nitapenda kumuenzi Yesu

“Lakini kamwe sitaacha kusaidia na kupenda watu kwa njia iliyosemwa na Yesu [Kristo].”

Hii ni kauli ya mwanamuziki maarufu duniani, Michael Jackson wa nchini Marekani.

By Jamhuri