JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Serikali, kampuni za simu kusaidia watoto, wanawake

Serikali imesema itaendelea kushirikiana na kampuni za simu ili kuwasaidia wananchi katika huduma mbalimbali za kijamii zikiwamo za afya, elimu na miundombinu. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Vodacom Tanzania Foundation hivi karibuni, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za…

Pongezi Tumaini Media, eneeni nchi nzima

Ni jambo la kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa hatua iliyofikiwa na Tumaini Media kuanzisha matangazo katika Jiji na Mkoa wa Dodoma. Kupitia Tumaini Media tunapata huduma nyingi za kiroho, kimwili na kijamii, ikiwa ni pamoja na uinjilishaji, kuelimisha umma kuhusu…

TPA inavyohudumia shehena ya mafuta, gesi

Katika mfululizo wa makala za bandari, wiki hii tunakuletea makala ya uhudumiaji wa shehena za mafuta na gesi katika bandari za Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), hususan katika Bandari ya Dar es Salaam. Shehena za mafuata huagizwa na…

Ndugu Rais tukiwachekea waliokosa maarifa nchi itaangamia!

Ndugu Rais sitakusahau kwa ‘kiki’ (msemo wa vijana wakimaanisha kukwezwa) uliyonitunuku ukiwa waziri mwenye dhamana ya barabara. Huku kwetu Mbagala-Kokoto wa zamani wanajua kuwa ni mimi niliyesababisha ujenzi wa barabara mbili kutoka Mbagala-Terminal zilipoishia hadi hapa kwetu Mbagala-Kokoto. Ukiwa msomaji…

Fikra inasaidia kuchochea maendeleo

Watanzania tuna kitu kinachotusumbua. Tunataka kujenga jamii iliyo bora. Tunataka kujenga jamii yenye mshikamano na uzalendo. Tunataka kujenga jamii yenye maadili mema na kuwarithisha watoto wetu maadili hayo. Tunataka kujenga jamii ambayo itarithisha vizazi vijavyo Tanzania yenye neema. Tutaijenga vipi…

Historia ya ukombozi inatoweka polepole

Juma liliopita nimeongozana na ugeni kutoka baadhi ya nchi za Kusini mwa Afrika – Namibia, Zimbabwe, Msumbiji, na Zambia –sehemu ya wajumbe wa bodi ya Southern African Research and Documentation Centre (SARDC), kituo cha utafiti kilichopo Harare kinachofanya kazi kwa karibu sana…