JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Prince Charles, JK wateta ujangili

Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Uingereza, Prince Charles, ambaye pia ni mtoto wa Malkia wa nchi hiyo, Elizabeth, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua zake za dhati za kulinda wanyamapori na kupambana na ujangili dhidi ya tembo na faru, taarifa ya Ikulu imesema.

KONA YA AFYA

Sababu za kupungua nguvu za kiume -3

Homoni ya kiume iitwayo testestorone, ambayo hutolewa na korodani husimamia kazi ya uume kama vile kuleta msisimko, hamu ya tendo la ndoa, kuchelewa kufika kileleni kiasi cha kufurahia tendo la ndoa.

Maswi: Gesi imeanza kuwatajirisha Mtwara

“Kazi ya kuunganisha na kusambaza mabomba ya kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam imefikia hatua ya kuridhisha. Kazi hiyo inafanywa na  mashirika yenye uzoefu mkubwa kimataifa, ambayo ni Shirika la Teknolojia na Mendeleo ya Petroli la China (CPTDC), Kampuni ya Kutengeneza Mabomba ya China (CCP), Worley Parsons Limited na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Tayari mpaka sasa kilomita 142 kati ya 542 zimekamilika. Mradi huo unaotarajiwa kukamilika Desemba mwakani na utakuwa na mitambo ya kisasa.”

Yah: Mheshimiwa Kikwete: wananchi wanasema yatosha!

Salamu nyingi sana kama mchanga wa pwani zikufikie mahali popote ulipo, hofu na mashaka ni juu yako uliye mbali na upeo wa macho yangu, na baada ya salaam je hujambo.

Rais anasubiri nini kuifumua Wizara ya Elimu

kama tujuavyo imebaki miaka miwili Rais aliyepo madarakani Jakaya Mrisho Kikwete amalize muda wake kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tayari tumemsikia Rais Kikwete akijivunia utendaji wake Amesema kwamba wale walioendelea kumsema vibaya kwamba chini ya uongozi wake Tanzania haikupata maendeleo  wataoona aibu atakampomaliza muda wake. Atakuwa ameiacha Tanzania ikiwa na maendeleo yasiyo na kifani.

Mwarobaini hutibu mnyauko wa migomba

Mwarobaini ni mojawapo ya mimea maarufu yenye kinga dhidi ya wadudu waharibifu. Ndani yake kuna dawa inayoweza kutolewa kwa urahisi na kutayarishwa na kutumika kama dawa ya mimea ya kuulia wadudu.