Latest Posts
Kuna ulimwengu mpya wa biashara
Hivi karibuni nilikutana na bwana mmoja mtaalamu wa masuala ya kompyuta, aliyenishawishi na kunishauri niwe na “application” kwenye “google play”. (Nimeshindwa kupata Kiswahili cha “Google Play” na “Application”). Kwa kifupi huu ni mfumo unaopatikana kwenye simu za “Smartphones, tablet na iPads”, ambao unakuwezesha kuwasiliana na kufanya biashara.
Ukraine yaivuruga Urusi
Vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea nchini Ukraine imeelezwa kutanuka na kusambaa nchini Urusi baada ya kiongozi wa upinzani, aliyepata kuwa Naibu Waziri Mkuu wa Urusi, Boris Nemtsov, kupingwa risasi mwishoni mwa wiki.
Warembo wa India, Nepal watumikishwa ngono Dar
. Uhamiaji yawanasa Mwananyamala Kisiwani
. Yawaokoa, wasimulia mateso makali ya jijini
. Walikuwa ni watu wa klabu tu, hawalijui jua
. Waliambiwa hapo Mwananyamala ni ‘Sauzi’
. Warejeshwa kwao, waliowaleta waadhibiwa
. Sasa waziponza klabu za Continental, Hunters
. Raha ndani ya klabu hizo sasa ‘zaota mbawa’
Kwa kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa mwaka jana (2014), wasichana 22 kutoka nchi za Nepal na India, walitumikishwa ngono na kufanyiwa vitendo vya kinyume na haki za binadamu.
Wavamizi wa ardhi wasifumbiwe macho
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanza kubomoa nyumba ambazo zimejengwa kwenye maeneo ya wazi na viwanja vilivyovyamiwa na watu wasio wamiliki halali wa viwanja hivyo.
Tutafakari vyema uamuzi wetu Oktoba
Unaweza ukajiuliza ni kwanini Ugiriki imeyumba vibaya kiuchumi? Sababu zipi za kiuchumi zilizoifikisha hapo ilipo?
Bosi NIC ang’olewa
* Bodi yakatisha mkataba ghafla
* Afika ofisini akuta kufuli mlangoni
* Mwenyewe adai umri wa kustaafu
Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Justine Peter Mwandu, sasa ameondolewa kazini akiwa amebakiza mkataba wa zaidi ya mwaka mmoja wa utumishi wake, imefahamika jijini Dar es Salaam.