Na Abel Paul wa Jeshi la Polisi-Dar es Salaam

Askari Polisi kutoka Ujeruman na Thailand wametoa uzoefu wao katika maswala ya Polisi jamii na namna ambavyo wanatoa huduma kwa jamii katika mataifa hayo ambayo yamejikita zaidi katika maswala ya Polisi Jamii.

Akiongea mara baada ya mafunzo hayo Profesa Krisanaphong Poothakool, kutoka Thailand amesema Polisi awezi kufanya kazi mwenyewe bila kushirikisha jamii ambapo amebainisha kuwa Polisi akiaminiwa na jamii ananafasi kubwa ya kupata taarifa.

Ameendelea kusema kuwa Polisi Watanzania wanayonafasi ya kufanya jitihada zaidi katika masuala ya Polisi jamii wanayofanya ili kupata kile wanachokita katika kutokomeza uhalifu.

Nae kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP URICH Matei ambae amemwakilisha kamishina wa kamisheni ya ushirikishwaji Jamii CP Faustine Shilogile amesema dira ya Polisi kwa sasa chini ya Mkuu wa Jeshi ni kushirikisha jamii katika kukabiliana na uhalifu Katika jamii ambapo ameongeza kuwa watumishi wa Serikali za mitaa kushirikiana na askari kata.

SACP Matei amewataka maofisa wanafunzi waliopata elimu hiyo na uzorfu kutoka kwa Polisi wa Thailand na Ujerumani kutumiwa vyema elimu waliyo ipata Kwenda kutoa huduma bora Zaidi kwa wananchi wanao litegemea Jeshi la Polisi.

Kwa upande wake Karl-Peter Schönfisch ambae ni mwakilishi wa Hanns Seideil Foundation amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania IGP Camillus Wambura kwa matokeo chanya wa mfumo wa Polisi jamii ambapo amesema wao wamejifunza vitu vizuri kutoka Jeshi la Polisi Tanzania kwa namna wanavyoshirikisha jamii kutatua uhalifu ambapo amebainisha kuwa wao wamekuwa wakishirikisha jamii bila ya kuwa na kamisheni inayohusika na Polisi jamii katika masuala ya Polisi jamii.

Nae mkuu wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam Dkt. Lazaro Mambosasa amewashukuru askari hao kwa kubadilisha uzoefu licha ya kuwa wao wako mbele kiteknolojia katika kukabiliana na uhalifu ambapo amebainisha kuwa wamejifunza vitu vingi ambavyo vitakuwa na faida kwa jamii na taifa kwa ujumla.

By Jamhuri