Na mwandishi wetu Jamhuri Media , Doha Qatar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki uzinduzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Mboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ukumbini kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.


Maonesho hayo yanatoa fursa kwa wafanyabiashara na wajasiriamali kujifunza na kuwekeza katika kilimo hususan kwenye teknolojia rafiki ya mazingira.

Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa nna Mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu Zuhura Yunus leo Oktoba 02, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na Amiri wa Taifa la Qatar Mhe. Sheikh Tamim Bin Hamad Al-Than wa pili kutoka kushoto kwake pamoja na viongozi wengine wakati wa Wimbo wa Taifa wa Qatar ukiimbwa kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) uliofanyika Doha tarehe 02 Oktoba, 2023.


“Maonesho haya yanafanyika wakati dunia inakabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi na uhaba wa chakula.” Amesema Zuhura


Amesema,ili kupambana na hali hii uwekezaji wa mitaji kwenye sekta ya kilimo hasa sekta hiyo ndogo ya mboga na matunda imeonekana kuwa na umuhimu ili kuongeza usalama wa chakula duniani na kutunza mazingira kwa wakati mmoja.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.


Serikali ya Tanzania kupitia taasisi zake mbalimbali na sekta binafsi itashiriki katika maonesho haya kwa lengo la kutafuta masoko ya mazao ya kilimo.


Tanzania ni moja ya nchi za Afrika ambazo zimekuwa zikijitosheleza kwa chakula na sasa imeweka msukumo mkubwa kwenye uwekezaji wa kilimo hasa eneo la upatikanaji wa mbegu bora, miundombinu ya umwagiliaji, utafiti pamoja na upatikanaji wa mbolea nafuu na viuatilifu.
Juhudi hizi zinalenga kupunguza gharama za uzalishaji kwa mkulima na kuongeza tija na uzalishaji kwa ajili ya kutosheleza mahitaji ya ndani na ziada kuuza nchi nyingine.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.


Sekta ya mboga na matunda ni miongoni mwa sekta zinazokua kwa kasi kwa mwaka kati ya 7% hadi 11% na kutoa fursa za ajira kwa takriban watu milioni 6.5 hasa kwa vijana na wanawake.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.
Shamrashamra za Ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.
Shamrashamra za Ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.


Shamrashamra za Ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kilimo cha Mbogamboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) nchini Qatar tarehe 02 Oktoba, 2023.