ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), Taifa na baadaye akawa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita amefariki dunia leo Alhamisi, Septemba 13, 2018 alfajiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na mdogo wake na marehemu, Gerald Guninita ambaye naye aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo wakati wa Uongozi wa Awamu ya Nne.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja Muhimbili, Aminiel Aligaesha amesema kwamba, Guninita amefariki dunia leo saa 12 asubuhi na alilazwa Muhimbili tangu Septemba 6, mwaka huu.

Mnamo Agosti 14, 2015, John Guninita na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja walihamia Chadema wakati wa vuguvugu la uchaguzi mkuu wa mwaka huo lakini baadaye Guninita alirejea tena CCM.

By Jamhuri