๐๐๐ฉ๐๐๐ช ๐๐ ๐ช๐ช ๐ฟ๐ ๐ฉ. ๐๐๐๐๐ง๐ค ๐๐ฌ๐๐ฅ๐ค๐ ๐๐ ๐๐๐ค๐ฃ๐๐ค๐ฏ๐ ๐ฌ๐ ๐พ๐๐ผ๐ฟ๐๐๐ผ ๐ฃ๐ ๐ผ๐พ๐
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro amewapokea wanachama watatu (3) ambao mmoja ni Kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na wawili wa ACT Wazalendo wote wa Mkoa wa Manyara, leo tarehe 4 Oktoba 2025.
Dkt. Migiro amewakaribisha wananchama hao katika mkutano wa kampeni wa Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. ๐ฆ๐ฎ๐บ๐ถ๐ฎ ๐ฆ๐๐น๐๐ต๐ ๐๐ฎ๐๐๐ฎ๐ป, uliofanyika katika Uwanja wa Stendi ya zamani ya mabasi ya Babati, mkoani Manyara.
Wanachama hao ni aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Simanjiro kwa tiketi ya ACT Wazalendo Bw. Olekai Letion Laizer, Aliyekuwa Katibu wa Ngome ya Vijana ACT Wazalendo Simanjiro Bw. Daniel Lucas Pamoja na Bw. Abubakari Abdalah, aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Babati Mjini na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa kupitia chama hicho.
Wakizungumzia sababu za kuhamia CCM, wanachama hao wamesema kuwa ni kutokana na kazi kubwa ya kuleta maendeleo kwa Watanzania na Taifa kwa ujumla lakini kuepukana na upinzani usio wa staha wenye kupandikiza chuki, kuhamasisha vurugu, kebehi na matusi na wenye kuweka mbele maslahi binafsi badala ya Taifa na kuwa na uzalendo.






