Wakenya wanavyoziua Serengeti, Loliondo

Baadhi ya wageni hao wamediriki kuendesha shughuli za ufugaji katika Hifadhi ya Taifa Serengeti (SENAPA), na kilimo katika vijiji vya Tarafa ya Loliondo. Matrekta mengi yanayotumiwa katika kilimo eneo la Loliondo yanatolewa Kenya.

JAMHURI limepata majina zaidi ya 280 ya Wakenya wanaoishi Ngorongoro, ambao baadhi yao wamekimbia wakihofu uongozi mpya wa Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli.

Pamoja na kuingia hadi SENAPA, Wakenya hao wamekuwa wakinunua mashamba na kuendesha kilimo katika Pori Tengefu la Loliondo na hivyo kuhatarisha uhifadhi katika eneo hilo.

Utambuzi wa wageni hao umekuwa mgumu kwa vile hawana tofauti ya ki-mwonekano na hata lugha na wenzao wa Tanzania. Viongozi kadhaa wa Tanzania wanatuhumiwa kuwapokea na kuwalinda.

Imebainika kuwa miongoni mwao wanajihusisha moja kwa moja kwenye uanzishaji na uendeshaji wa asasi zisizo za serikali (NGOs) ambazo zimekuwa ndiyo ‘watalawa’ wa Loliondo kwa kivuli cha utetezi wa wafugaji.

Kwa kutumia mashirika hayo, wamefanikiwa kuwa na ukwasi mkubwa wa kifedha kupitia ufadhili; na wakati huo huo kuutumia mwanya wa utetezi wa wafugaji kuingiza maelfu ya mifugo kutoka Kenya.

Mwaka jana sehemu ya mifugo hiyo iliyokuwa ndani ya SENAPA iliondolewa baada ya kazi kubwa iliyofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Hashim Shaibu.

Uchunguzi wa JAMHURI umebaini kuwa wahamiaji na walowezi hao haramu wengi wao wanaishi na kuendesha shughuli katika kata za Engaresero, Orgosorok, Oloipir, Oloirien-Magaiduru, Oloosoito-Maaloni na Ololosokwan.

Kuwapo kwa Wakenya hao Loliondo kunatajwa kusababisha athari nyingi za kiusalama na kiuchumi. Athari hizo zinaonekana wazi katika eneo la Wasso ambako mamia ya wageni wamemilikishwa ardhi na kujenga nyumba za kuishi na za kibiashara.

Katika Kijiji cha Ololosokwan, Wakenya hao wapo katika vitongoji vya Osero Sopia, Eng’ong Nairouwa (Maji Moto), Kururu, Olorien, na Enting’iting.

Operesheni iliyoendeshwa hivi karibuni na vyombo vya ulinzi na usalama katika Wilaya ya Ngorongoro ilibaini Wakenya zaidi ya 60 wenye maelfu ya ng’ombe, mbuzi na kondoo ndani ya SENAPA. Wafugaji hao wa kigeni walikutwa hadi kilometa 10 ndani ya Hifadhi hiyo yenye umaarufu wa kipekee duniani.

DC Hashim, amezungumza na JAMHURI na kusema pamoja na vikwazo anavyopambana navyo, amehakikisha anapunguza tatizo la wahamiaji haramu ambalo anasema lilishaota mizizi.

“Nipo hapa kuyatambua na kuyalinda maslahi ya Tanzania na wananchi wa Tanzania. Hatuwakatai wageni, lakini wanapaswa waingie nchini na kufanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi yetu. Kazi hii ni ngumu, lakini nashukuru napata ushirikiano kutoka kwa vyombo vyote,” amesema Hashim ambaye kwa muda mfupi aliokaa Ngorongoro amenyoosha mambo mengi.

Amesema baadhi ya watu waliotambuliwa kuwa ni Wakenya wamesharejeshwa kwao kwa kufuata sheria na taratibu za kitaifa na kimataifa.

Uchunguzi wa JAMHURI umefanikiwa kuwatambua wavamizi hao. Majina yao na maeneo wanakotoka nchini Kenya ni kama ifuatavyo:

1: Moiyare        Laleta   

2: Ole Kairung’u (Naikara)        

3: Zakaria Narikay   (Embash)

4: Ole Nkai Kapiro (Kenya)    

5. Ole Toroge Naikara

6: Ole Shunguru (Embash)  

7: Ole Kirigany        (Ngusero Sambu, Tanzania)             

8: Oloosekenge Reiya (Embash)

9: Ole Engo     (Losekengei)      

10:  Ole Rikaiyan (Esoit)    

11: Ole Nkuruna (Olderkesi)     

12: Olorgeso (Embash)      

13: Ole Koikai (Naroosura)

14: Ole Kimojino (Naroosura)   

15: Ole Naing’isa (Naroosura)   

16: Ole Ngiminisi    (Naroosura)

17: Ole Rakwa (Naroosura)       

18: Ole Ketuta (Kipaipaya       )  

19: Ole Lindi   (Engusero Sambu, Tanzania)             

20: Ole Ndaiya (Naroosura)      

21: Ole Kinayio (Naroosura)     

22:   Ole Leitepa (Pusumoru)  

23: Ole Koiyiee (Engusero Sambu, Tanzania)    

24: Kimaa        (Enkoiroroi)      

25: Ole Silandoi Naroosura Ole

26: Ole Reiyia (Esoit)

27: Ololoso (Lesekengei)

28:   Ole Kinayio Odoo (Naroosura)      

29: Orkokoyoi Oloinyo (Olalaimutia)

30: Ole Kikonya (Olderkesi)      

31: Ole Kursai (Talek)  

32: Ole Kikonya (Olderkesi)

33: Ole Pirikanyi (Lalaimutia)    

34: Ole Letoluo (Noonjutaa)

35: Ole Mayiani (Oldekesi)

36: Ole Ngurunaa (Posimoru)   

37: Ole Sakerini (Losho)    

38: Ole Murunya (Oldekesi)               

39: Ole Kioko (Orkiloriti)          

40: Ole Kariboloo (Oldekesi)     

41: Ole Shukur (Oldisare)  

42: Ole Naingisa (Mosiro)         

43: Ole Ketuta (Telegutu)          

43:   Ole Kinayio (Osupuko) Ole

44: Ole Mundere (Naikaraa)      

45: Ole Karia (Noonjuta)

46: Ole Kasoe (Olorok)  

47: Miponyi Kipila (Lalamutia)          

48: Ole Motire (Osupuko)         

49: Nyakuni (Ngo’munisho)              

50: Ole Sarite (Osupuko)   

51: Ole Kindet (Lalaimutia)

52:  Ole Shunguru (Naroksuraa)        

53: Oldapash Masharehi (Engoilaleie)    

54: Maripet Purengei (Naroksuraa)    

55: Ole Koshal (Naikaraa)          

56: Ole Kasoe (Ematie)            

Baada ya kuondolewa ndani ya SENAPA, Wakenya hao na maelfu ya mifugo yao walihifadhiwa kwa muda katika maeneo ya Kilamben, Oloirien, Mederi/Kururu, Olooseke, Kokaa, Osero Sopia na Maji Moto.

Uchunguzi umebaini kuwapo kwa juhudi za viongozi waandamizi kutoka Kenya waliofika nchini na wengine kutuma ujumbe wakihaha ili mifugo hiyo iachiwe.

Wakenya wameanzisha Soko la Mifugo la Karkamoru katika Kata ya Oloipir huku viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro wakiwa hawajaliidhinisha. Mtetezi mkuu wa mnada huo anatajwa kuwa ni Diwani wa Soitsambu, Daniel Ngoitiko.

“Ni soko lililoanzishwa kwa nguvu za Wakenya. Halmashauri hailitambui wala hakuna ushuru unaokusanywa. Wanajaa Wakenya wanaouza na kununua ng’ombe. Wanaotetea ni baadhi ya viongozi ambao nao uraia wao una shaka,” kimesema chanzo chetu.

DC Shaibu, anakiri kuwapo wimbi kubwa la wahamiaji haramu na walowezi katika wilaya hiyo, na ahadi yake ni kwamba wataondolewa.

Katika kuthibitisha hilo kwa vitendo, amesimamia kufungwa baadhi ya maeneo ya mipakani ili kukabiliana na wimbi kubwa la wahamiaji hao ambao wamekuwa na athari kubwa kwa Loliondo na SENAPA.

Baadhi ya maeneo yaliyofungwa ni ya Ololosokwan kuelekea Posmoru ambako kuna mnada mkubwa wa mifugo unaohodhiwa na Wakenya.

DC Shaibu anasema: “Operesheni imefanyika, tumepata mafanikio makubwa. Raia 17 wa Kenya tumewakamata wakiwa na mifugo 3,510. Wengine 44 walikimbia na mifugo yao. Tuliowakamata tumewafikisha mahakamani. Tumeruhusu mifugo iachiwe kwenda Kenya. Viongozi wa Kenya wakiwamo machifu na ma-DC walifika Loliondo tukazungumza.

“Tukawambia wazi kuwa ujirani mwema ni muhimu, lakini siyo wa kuleta mifugo kuvuruga huku kwetu. Bado tunao Wakenya wengi ambao tunataka wafuate taratibu za kuishi nchini. Wananchi wetu tumeanza kuwapa elimu ili wajue athari za wahamiaji haramu. Wao wanajua hao wahamiaji ni ndugu zao, lakini tunawaambia hasara za kuwakaribisha bila kufuata taratibu na sheria. Tunaomba wananchi wote wawe wazalendo ili kulilinda Taifa letu.”

Hatua ya Shaibu ni mwendelezo wa maagizo ya Mkuu wa Mkoa (RC) na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda, ambaye kwa nyakati tofauti alinukuliwa akiapa kuhakikisha Loliondo inatawalika.

Ndibenda anatambua nguvu za wahamiaji na walowezi na namna wanavyotumia nguvu za fedha kupitia NGOs ili kuhakikisha Loliondo na Ngorongoro zinakuwa kwenye migogoro kwa muda wote.

Mwaka jana, aliyekuwa Diwani wa Ololosokwan, Yanik Ndoinyo, alizungumza na JAMHURI na kukiri kuwa msako mkali ulifanywa na vyombo vya ulinzi na usalama na kuwanasa raia kadhaa wa Kenya. Kata ya Ololosokwan inatajwa kuwa miongoni mwa maeneo yenye Wakenya wengi.

Kamishna wa Huduma za Uhamiaji na Udhibiti wa Mipaka, Abudallah Abdullah, amesema suala la kuwashughulikia wahamiaji haramu na walowezi katika Wilaya ya Ngorongoro limeanza na ni la kudumu.

Wamiliki ardhi kubwa

Ingawa sheria za ardhi za Tanzania zinazuia raia wa kigeni kumilikishwa ardhi, walowezi na wahamiaji haramu wanamiliki aradhi kubwa katika vijiji vya Soitsambu na Ololosokwan.

“Hapa wana ardhi kubwa kwa sababu walikotoka wanajua thamani ya ardhi. Wamefanya watu wetu wakose malisho na kwa sababu hiyo kuna migogoro ya mara kwa mara.

“Tumekuwa na vikao vya kulaani vitendo vyao vya kutaka kukigawa kijiji na wakati vikao hivyo vimesimamiwa na wazee wa mila. Umiliki wa ardhi wameupata kutokana na wao kushika nafasi katika uongozi wa kata na vijiji wao wenyewe au kwa kuwaweka wenzao wenye asili ya Kenya. Utaona hata Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka jana waliingia, lakini wakawekewa pingamizi. Mbaya zaidi wanaingia CCM ambako wanajua hawataguswa,” anasema mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la ole Sipai.  

Uchunguzi wa JAMHURI unaonyesha kuwa wakati wa uchaguzi watuhumiwa kwa kiasi kikubwa waliingiza Wakenya wenye mifugo katika ardhi ya kijiji na kuingiza magari kutoka Kenya kwa ajili ya kuwasaidia wao na watu wao katika kampeni.

Moja ya magari aliyokuwa anatumia mmoja wa watuhumiwa ni Toyota Land Cruiser lenye usajili wa Kenya wa namba KAM 591 J.

Mtandao wao unatajwa kuwa wenye nguvu kwani hata Jeshi la Polisi, licha ya kuwa na taarifa za uhakika juu ya matukio hayo, halichukui hatua. Lawama zinaelekezwa kwa polisi wa Kituo cha Ololosokwan.

ORODHA YA WAHAMIAJI HARAMU WAKENYA WANAOISHI LOLIONDO NA KUIVURUGA SENAPA

Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI katika vijiji kadhaa katika Tarafa ya Loliondo umebaini majina 224 ya Wakenya ambao, ama ni wahamiaji haramu, au walowezi. Wakenya hao wanaishi na kuendesha shughuli zao huku wakipata haki zote kama Watanzania halali. Majina ya Wakenya hao ni:

1: Peter Kiromo

2: Elizabeth Nairushiye

3: Kennedy Manyeki

4: Katikasha Kamanga

5: Risa Kamanga

6: Huho Daniel

7: Jackson Manyeki

8: Glady Kurgat

9: Elizabeth Ongetont

10: James Koromo

11: John Nzuna

12: Anna Ramasigonde

13: Omaria Lengaaki

14: Nangaya Lengaaki

15: Ndito Lengaaki

16: Kalee Saitabau

17: Najara Koleli

18: Joshua Saitabau

19: Timan Rika Yion

20: Ngopeesho Olekorkai

21: Ngisu Olenanyokie

22: Joel Siyianga

23: Sikemboi Sisi

24: Noosokono Koleli

25: Lasaru Saitabau

26: Noorkorea Sisi

27: Olemeen Ngoikor

28: Joel Lengaaki

29: Elija ole Matian

30: Joel Siyanka

31: Parkipoi Murera

32: Iman Olemetian

33: Nangida Olemen

34: Joshua Mwarabu

35: Oloibor Ngapai

36: Andrew Nkanuma

37: Sintako Nkanuma

38: Ngaina Saitabau

39: Nosilat Naingisa

40: Susana Massago (mama)

41: Binifas Massago

42: Oloongoshoka Ndaiya

43: Lengoko Saitabau

44: Modolu Yengo

45: Sirere Mpoe

46: Oleengot Engo

47: Oletimoi Stephen

48: Joshua Marabui

49: David Sais

50: Lekakiuy Sananka

51: James Massago

52: Bebi Massago

53: John Ngile

54: Ole Kileu

55: Ole Sasii

56: Joel Karori

57: Chuma Shambarao

58: Olooseenge Rea

59: Sakaria Narikai

60: Orandaya Kitipa

61: Alex David

62: Dopoi Kitipa

63: Kosia David

64: Porosooi Ndaiya

65: Boma ya Oleshung

66: Boma ya ole Serei-Kututuo

67: Boma ya Olekitipa

68: Nganuma Lemorara

69: Nganeni Lemorara

70: Ng’onene Nkanuma

71: Anna Gathu

72: Ruth Kabulunze Musomba

73: David Marko Sessat

74: Naomi Marko Sessat

75: Josephine Kuria

76: Joseph Kabulunze Musomba

77: Elizabeth Musumba

78: Marco Muhinge

79: Christine Musomba

80: Ndolee Temwee

81: Jane Koromo

82: Philipo Justus Marco

83: Pareyo Kitipa

84: Olengutie Saing’eu

85: Lekinyit Reyia

86: Esophie Parmat na ndugu zake

87: Kararit Ndaiya

88: Peter Kashal

89: Olemundere

90: Kisarunga Leitura

91: Luthia Ngelenche

92: Christine Francis William

93: Christopher Marco Sessat

94: Denis Okirigiti

95: Aizack Tura

96: Magreth Kiromo

97: Peter Robert Kiromo

98: Steven Kabulunje (dereva Hifadhini)

99: Peter Mtune Kaput

100: John ole Keroto

101: Siminde Lonyori

102: Anna Ngelenche

103: Zakayo Sesat

104: Pius Mtune Kaput

105: Emmanuel Samwel

106: Joseph Sessat

107: Estomih Manyeki

108: Joachim Manyeki

109: Felomona Mtune Kaput

110: Godfrey Kiromo

111: Godwin Mtune Kaput (Mwalimu Halmashauri)

112: Lazaro Sessat

113: Beatrice Kimoro

114: Evaline Bilechi

115: Saimon Sessat

116: Emmanuel Sassat

117: Lucy Chambii

118: George Mtune Kaput

119: Yasinta Dunya

120: Anna Cheburge

121: Joyce Marko

122: Elizabeth Robert

123: Mamiam Koira

124: Lilian John

125: Josephine Koillah

126: Sananga Cooss

127: William Sangupa

128: Coos

129: Olekoreko

130: Amos Olekoreko

131: Joseph Olekoreko

132: Joseph Sessat

133: Mery Kuyato

134: Joseph Kipkia

135: Gudito Nyange

136: Marco William Mabwa

137: Yeremia Olekoreko

138: Napirura Olengopiri

139: Mapena Olengopiri

140: Manina Olenanyika

141: Kiparian Manina

142: Emmanuel Mtune Kaput

143: Nayeilo Angangi

144: Ndina Manina

145: Moris Manina

146: Soinkei Olekumbe

147: Naaramataki Olekumbe

148: Saaloi Leshashi

149: Langoi Leshashi

150: Sabina James Kiromo

151: Rozi Kiromo

152: Lourence Kiromo

153: Emmanuel Kiromo

154: Ateiti Sumare

155: Orkedienye Kapiro

156: Saruni Ngurumwa

157: Sanare Koshara

158: Kisoku Karbolu

159: Memus Sadira

160: Nanjiko Shukur

161: Kipuri Karbolo

162: Nginandei Melejeki

163: Makoi Melejeki

164: Kanaya Karbolo

165: Napatao Meyane

166: Maripet Purengei

167: Oloishuro Kariro

168: Oleshololoi

169: Kingorosh Manatiny

170: Frank Mtune Kaput

171: Kanai Mbatiany

172: Kashing Pikoyan

173: Naingei Koikay

174: Simore Letuluko

175: Nareyo Olekandika

176: Oleniboo

177: Michael Kitipa

178: Kayo Kitipa

179: Korema Mako

180: Shukuru

181: Olonyikid Sironike

182: Olokose Kapiro

183: Karungu

184: Moriko Ngurumwa

185: Shinga Mboe

186: Olorupa Pere

187: Sangau Mbatiany

188: Kararinyayia

189: Olesironik

190: Molinge Oloso

191: Orkelese Ndaiya

192: Ntumaini Nkanuma

193: Nteetu Nkanuma

194: Kosiando Tuke

195: Sopiya Kosiando

196: Daudi Mtune Kaput

197: Juliana Mtune Kaput

198: Francis Mabwa

199: Yohana Sessat

200: Saitoti Kosiando

201: Tina Leshana

202: Shirimu Kuya

203: Ndooriti Koleli

204: Ngicha Oleneko

205: Musu Ngicha

206: Lonyokie Ngicha

207: Tiene Ngicha

208: Titio Ngicha

209: John Kamanga

210: Mbizi Ololeng’a

211: Olengaiki Olepombo

212: Joseph Siere

213: Melejeki Olemunya

214: Saitoti Ngekee

215: Lesidai Melejeki

216: Koika Melejeki

217: Mbaayi Kosiando

218: Ndima Kosiando

219: Koleli Lesite

220: John Koleli

221: Kijooli Melejeki

222: Esophip Parmwat

223: Marco Parmwat

224: Kunday Parmwat