Waziri Mkuu wa Palestina, Mohammad Shtayyeh ametangaza kujiuzulu.

Akitangaza uamuzi huo leo, Shtayyeh amesema uamuzi huo unatokana na serikali yake kutawala sehemu za Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.

“Ninawasilisha kujiuzulu kwa serikali kwa Rais (Mahmud Abbas),” Shtayyeh amesema, na kuongeza kuwa inakuja kutokana na vurugu katika Ukanda wa Gaza na kuongezeka kwa Ukingo wa Magharibi na Jerusalem.

“Ninaona kwamba hatua inayofuata na changamoto zake zinahitaji mipango mipya ya kiserikali na kisiasa ambayo inazingatia ukweli huko Gaza na haja ya makubaliano ya Palestina kulingana na umoja wa Palestina.” aliongeza.

By Jamhuri