Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  akizungumza na wagonjwa waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Amana kwa ajili ya kupatiwa matibabu wakati alipofanya ziara ya kukagua hospitali hizo mara baada ya Rais Dk John Pombe Magufuli kuagiza Hospitali hizo zianze kusimamiwa na Wizara ya Afya.
 Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Amana, Dr Meshack Shimwela  akitoa maelezo kwa Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu, akikagua katika ubao wa Matangazo  ambao unaonyesha namna ya watu wanatakiwa kuhudumiwa katika hospitali hiyo.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akizungumza na Wanawake ambao wamejifungua katika  Hospitali ya Rufaa ya  Amana
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akipokea maekezo kutoka kwa  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Amana, Dr Meshack Shimwela juu ya ujenzi wa jengo jipya la kuhudumia wagonjwa
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  akizungumza na Mmoja ya Wamama ambao wamelzwa na Watoto wao katika wodi mpya iliyojengwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda .

 
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  akikagua Dawa zilizopo katika Bohari ya Dawa ya Hospitali ya Rufa aya Amana Jijini Dar es Salaam.
 

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  akizungumza na Madaktari ndani ya Wodi ya watoto katika Hospitali ya Amana.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  akikagua Majengo ya Hospitali ya Amana.
WAZIRI  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu  amesema kuwa kuna changamoto ya uhaba wa madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Amana jijini Dar es Salaam kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaofika kwa ajili ya kupata huduma katika hospitali hiyo.
Ametoa kauli hiyo leo wakati anamalizia ziara yake kwenye hospitali hiyo ambapo amesema pamoja na kuridhishwa na huduma ambazo madaktari wanazitoa kwa wagonjwa katika hospitali hiyo lakini bado kuna changamoto ya uhaba wa madaktari.”Nimeridhishwa na huduma katika hospitali hii na nimpongeze Mganga Mfawidhi na uongozi  wa Wilaya  kwa kazi nzuri wanayoifanya licha ya kwamba bado tunafahamu kuna changamaoto katika sekta ya afya.
“Madaktari wa Amana kwa siku wanahudumia wagonjwa 800 , hivyo tunachangamoto ya uhaba wa madaktari na kwa kuwa kuna nafasi za ajira 52,000 zimetangazwa tunaamini sekta ya afya tutapewa mgao unaostaili ili tuwe na wataalamu wa masuala ya afya wa kutosha,”amesema Waziri Mwalimu.Mbali ya changamoto ya uhaba wa madaktari, Waziri Mwalimu ameendelea kuwasisitiza wagonjwa umuhimu wa kuwa na kadi za bima ya afya kwani humfanya anayekuwa nayo kuwa na uhakika wa kupata matibabu kwa gharama nafuu.
“Ifike wakati kila mwananchi awe na kadi ya bima ya afya kwani milango imefunguka na kilichobaki ni kuendelea kuona umuhimu wa kuwa nayo,”amesema Waziri Mwalimu.Wakati huohuo ametoa onyo kwa watumishi wote wa hospitali za Serikali ambao watabainika kujihusisha na tabia ya kuuza dawa ambazo zimetolewa na Bohari ya Dawa(MSD)ambazo zinatolewa bure waache mara moja.

By Jamhuri