Klabu ya Barcelona, imetwaa ubingwa wa kombe la Super Cup,kwa kuifunga Sevilla kwa magoli 2-1 katika mchezo uliochezwa nchini Morocco.

Sevilla ndio walianza kuzifumania nyavu za wapinzani wao kwa kufunga goli ka kuongoza katika dakika ya tisa ya mchezo kupitia kwa mchezaji wake Pablo Sarabia.

Beki kisiki wa Barcelona, Gerald Pique, akasawazisha goli hilo katika dakika ya 42 ya mchezo, winga wa Kifaransa Ousmane Dembele, akaifungia timu yake bao la ushindi katika dakika ya 78.

By Jamhuri