Catalonia Yashinda Uchaguzi ya Kutaka Kujitoa na Uhispania

Vyama vinavyounga mkono jimbo la Catalonia kujitenga na Uhispania vimeshinda uchaguzi wa jimbo la Catalonia.

Ikiwa kura zote zinakaribia kukamillika kuhesabiwa Katika rekodi ya wapiga idadi ya wapiga kura ambao wamejitokeza vyama hivyo vinaonekana kushinda jambo kimepunguza kidogo idadi ya viti bungeni.

Matokeo hayo kwa vyovyote ni habari mbaya kwa waziri mkuu wa Hispania,Mariano Rajoy ambaye aliingilia kati jimbo hilo kujitenga hivi karibuni na kuitisha uchaguzi huo.

Akiwa uhamishoni mjini Brussels aliyekuwa rais wa Catalonia ,Carles Puigdemont amepongeza matokeo hayo na kusema ni ushindi wa demokrasia kwa sabbu idadi kubwa ya watu walijitokeza ,rekodi ya watu waliopiga kura na idadi ya waliojitokeza ndio iliyosababisha matokeo haya na hakuna anayeweza kuyapinga.

Hata hivyo baada ya uchaguzi huo tatizo kubwa kwa pande zote ni kwamba hakuna uhakika kuwa uchaguzi huo na matokeo hayo yanawea kutatua mgogori huo unaendelea baina ya Catalonia na serikali ya Madrid.