Category: MCHANGANYIKO
Brandts aliisubiri Simba kuwapumzisha wakongwe?
Kati ya mambo yaliyojadiliwa na wapenzi wa soka wiki iliyopita, ni pamoja na matokeo ya mechi ya watani wa jadi — Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club (Mnyama) ya jijini na Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake mitaa ya Jangwani na Twiga, baada ya timu hizo kutoka sare ya mabao 3-3 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa katika Dimba la Taifa Dar es Salaam.
Ubaguzi wa rangi washika kasi Ulaya
Kuna kila hali inayoonesha kuwa kwa sasa vitendo vya ubaguzi wa rangi, vinazidi kushika kasi katika soka barani Ulaya, pamoja na kuwa kumekuwa na kampeni za hapa na pale za kupiga vita dhidi ya vitendo vya ubaguzi.
Dola yatuhumiwa kwa mauaji Tabora
Kumekuwa na matukio ya mauaji ya watu mara kwa mara katika wilaya za Urambo na Kaliua mkoani Tabora, yanayofanywa na baadhi ya watendaji wa vyombo vya dola, hali inayoendelea kutishia maisha ya watu, huku ikionesha kuwa hakuna hatua za kuridhisha zinazochukuliwa kukabili tatizo hilo.
Wanahangaikia urais 2015, TAMWA waokoe wanawake mkoani Dodoma
Nchi yetu kwa sasa imegeuka taifa la uchaguzi. Ukipita kwenye vijiwe vya kahawa, makao makuu ya vyama vya siasa, na hata hii Katiba mpya inayoandaliwa kila mtu analenga uchaguzi mwaka 2015. Tanzania ni nchi pekee kati ya nchi ninazozifahamu duniani, iliyojenga utamaduni wa kumaliza uchaguzi wanasiasa wakaanza harakati za uchaguzi unaofuata miaka mitano ijayo.
Yah: Kama mimi ningelikuwa Manumba ama wasaidizi wake?
Sasa hivi napenda nikiri wazi kwamba kama kuna mtu ama wana wakati mgumu wa kuingalia rediocall ama kusikilizi simu zao za mikononi za kikazi na siyo kindugu ama urafiki hawana muda wa kuangalia televisheni na kusikiliza redio basi ni kundi zima la Manumba mwenyewe na hao RCO wake wote, poleni lakini ndio kazi mliochagua kutokana na masomo yenu.
Dogo Aslay afurahia maisha ya muziki
Staa wa Bongo katika muziki wa kizazi kipya Aslay Isiaka, ‘Dogo Asley’ ambaye makazi yake ni jijini Dar es Salaam amesema kuwa sasa anfurahia maisha ya muziki kutokana na maendeleo aliyoyapata.