Chongolo ajionea kero ya ukosefu wa daraja Nguyami

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Daniel Chongolo akizungumza na wananchi wa Vijiji vya Mkwajuni na Ilalo mara baada ya kujionea kero kubwa ya kukosekana kwa daraja katika mto Nguyami linalounganisha vijiji hivyo viwili wilayani Gairo mkoa wa Morogoro.(Picha na CCM Makao Makuu)
Mtoto Tefa Adua (4) akivuka mto Nguyami ambapo kwa karibia miaka minne sasa wananchi wa kijiji cha Ilalo wamekuwa wakipata tabu baada ya daraja la awali kuharibika. (Picha na Adam H. Mzee)