Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko leo Agosti 3, 2023 jijini Dodoma amekutana na uongozi wa juu wa Kampuni ya Sotta Minerals Corporation Limited ambayo ni ya ubia Kati ya Serikali na kampuni ya Orecorp Tanzania limited ya Australia inayosimamia Mradi wa uchimbaji madini ya dhahabu uliopo wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.

Kupitia Mkutano huo, kampuni ya Sotta imeeleza maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwaka 2025.

Aidha, Dkt. Biteko ameelezwa kuwa, hivi sasa kampuni iko kwenye hatua za mwisho za kuweza kuwalipa fidia wananchi walio ndani ya eneo la mradi ili kuwezesha mradi huo kuanza.

By Jamhuri