Na mwandishi Wetu Jamhuri Media

Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu  Duniani (FIFA) amelitaka Shirikisho la Mpira wa miguu Barani Afrika (CAF) kuangalia upya kanuni la goli la ugenini kwa kuwa linaunyima uhalali wa usawa wa point na usawa wa idadi ya magoli kwa kila timu inayopambania fainali.

Rais huyu ameyasema haya baada ya mshindi wa mashindano ya kombe la Shirikisho la Mpira wa miguu Barani Afrika (CAF) kutangazwa katika fainali zilizomalizika Jana huko Nchni Algeria.

Maana mshindi aliye tangazwa ambaye ni timu ya US Alger amepata point 3 na magoli 2 Sawa kabisa na timu iliyokuwa ikishindana naye ambayo ni timu ya Dar Yanga African ambayo nayo imepata Point 3 na magoli 2 Sawa kabisa na aliuetangazwa kuwa Bingwa.

Mfumo huu ni Sawa na ule uliyokuwa ukitumika hapo Zamani wa kumpata Bingwa kwa kurusha shiringi na mchezeshaji.

Mifumo ya aina hii ilishaondoshwa kutumiwa kwenye mashirikisho mengi ya Mpira wa miguu Duniani isipokuwa Shirikisho la Bara la Afrika pekee.

Hivyo Shirikisho la Mpira wa miguu Duniani (FIFA) linatoa elekezo kwa Shirikisho la Mpira wa miguu Barani Afrika (CAF) kuangalia upya kanuni hii ili kuendana na kanuni za Mpira wa miguu Duniani ya kumpata Bingwa kwa uwingi wa point au uwingingi wa magoli ya kufunga.

Kwa matokeo ya hayo timu ya Dar Yanga African kutoka Tanzania ilistahili nayo kutangazwa kuwa Bingwa wa mashindano haya kama ilivyotangazwa timu ya US Alger kuwa ndiye Bingwa kwa kanuni kandamizi kama hii iliyobaki inatumiwa na Shirikisho la Mpira wa miguu Barani Afrika (CAF).

By Jamhuri