KAULI ZA WASOMAJI

Nasikitika vijana kukosa kazi

Ninasikitika kuona vijana wengi wasomi hapa Tanzania wakikosa kazi kwa muda mrefu baada ya kuhitimu masomo. Mikopo inayotolewa hairudishwi kwa wakati kwa sababu vijana hawana vyanzo vya mapato. Hivyo serikali itutafutie ufumbuzi wa tatizo hili kwa kasi, nguvu na ari mpya ili maisha bora kwa kila Mtanzania yapatikane.

 

Salim Habib, Morogoro

0652 054 343

JWTZ pumzikeni kwa amani

Askari wa JWTZ mliokufa kishujaa mkilinda amani nchini Sudan pumzikeni kwa amani. Natoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa wapiganaji hao. Ninaomba hayo malipo ya Sh milioni 100 yawafikie walengwa, hasa wajane na watoto wa askari hao, angalao yanaweza kuwasaidia.

 

Anko Mgingi Mhochi, Musoma

 

Serikali yetu ikubali kukosolewa

Viongozi wengi wa serikali ni wazushi, na wanataka kusifiwa siku zote, wanapokosolewa huanza kusingizia magazeti kwamba yanaandika uongo na kukipendelea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Mimi nawashauri viongozi wa aina hiyo wawe wanakubali kukosolewa.

 

Aziz Msafiri, Dodoma

0757 100 079

 

Viongozi kuweni na huruma

Viongozi mliokabidhiwa dhamana ya kuhudumia wananchi muwe na huruma. Mmeshindwa kupeleka walimu wenye vipaji katika Shule ya Sekondari ya Ngarenaro iliyopo kata ya National Housing. Naomba mshughulikie tatizo hilo jamani.

 

Mwananchi, Arusha

0756 253 900

 

Halmashauri Bariadi inanyanyasa watumishi

Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi imekithiri vitendo vya ukiritimba, rushwa na upendeleo katika utoaji wa ruhusa kwa watumishi, hasa walimu wanaohitaji kwenda kujiendeleza kielimu na kitaaluma. Mkurugenzi na Afisa Elimu katika halmashauri hii ni kikwazo kikubwa.

 

Msomaji wa JAMHURI, Bariadi

0716 138 159

 

Watanzania tufungue macho tuone

Watanzania tunapaswa kufungua macho tuone jinsi wabunge wetu wengi wasivyowajali wapigakura, badala yake wamekuwa viongozi wa kushabikia mambo yanayowakandamiza wananchi, badala ya kutetea maslahi ya umma.

 

Mpenzi wa JAMHURI

0754 516 966

 

Nimeona taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa ndugu Samuel Sitta anahoji uhalali wa Lowassa kupita kwenye nyumba za ibada. Najiuliza maswali haya: (a) Anahoji kama nani? (b) Anahoji kwa nia gani? (c) Yeye ni msafi kwa kiwango gani mpaka ahoji wengine?

 

Msomaji

0752 633 555

 

Taifa langu. Taifa ambalo mabinti wakimwona Mzungu wanadhani ana hela, taifa ambalo ukiongea Kiingereza unaonekana umesema sana, taifa ambalo ukiwa na simu nzuri we mjanja japo vocha unaweka jerojero, taifa ambalo waliofeli wanakuwa walimu/polkisi, taifa ambalo mtu kwao hawana umeme ila analalamika Tanesco wanaboa, taifa ambalo warembo wameshaona wao ni wa kupewa daima, taifa ambalo vijana wanalalamika hawana, ukimpa dili anaanza longolongo, taifa ambalo ukiwa na gari hutongozi ukitoa lifti tu baaaas, taifa ambalo mwanafunzi anafaulu huku hajui kusoma wala kuondika. Nalipenda taifa langu.

 

0712 813285