Mapacha walioungana (Maria na Consolata) wamefariki dunia usiku huu wa Jumamosi Juni 2, 2018 katika hospitali ya Iringa walikokuwa wakitibiwa.

Mapacha Hawa walifanikiwa kuanza masomo yao ya juu katika Chuo Kikuu Katoliki cha Ruaha (Ruco) cha mjini Iringa mwaka jana baada ya kufaulu vizuri masomo yao ya kidato cha sita.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini mkoani Iringa, Richard Kasesela amethibitisha kupkoea taarifa za msiba huo.

Tangu mwishoni mwa mwaka jana, mapacha hao walifanyiwa uchunguzi mara kadhaa baada ya kupata matatizo ya moyo.

 

Mapacha hao waliwahi kulazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya Matibabu wakitolewa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Iringa.

 

Katika safari ya elimu, Maria na Consolata walionesha uwezo mkubwa tangu walipohitimu na kufaulu Darasa la Saba mwaka 2010 katika Shule ya Msingi ya Ikonda wilayani Makete, baadaye walijiunga na Kidato cha Nne katika shule ya Sekondari ya Udzungwa iliyopo Wilayani Kilolo

Walisoma pia kidato cha 5 na 6 katika shule hiyo na baadaye walijiunga na Elimu ya Juu katika Chuo Kikuu cha Ruaha(RUCU) baada ya kupata daraja la 2 katika mtihani wa Kidato cha 6

Maria na Consolata walizaliwa katika Hospitali ya Misheni ya Ikonda wilayani Makete mkoani Njombe mwaka 1996.

 

Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za wapendwa wetu mahali pema peponi, Amina.

 

By Jamhuri