Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb.), amewasili mkoani Shinyanga kwa ziara maalum ya kikazi ya kukagua utekelezaji na kuzindua miradi ya maendeleo, pamoja na kuzungumza na wananchi katika wilaya za Mkoa wa Shinyanga.
Waziri Ndejembi, ambaye ni Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, mara baada ya kuwasili amefika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Mboni Mhita, tarehe 09 Agosti 2026.
Waziri Ndejembi akiwa mkoani hapo, atakagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Kahama – Kakola, mradi wa ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama, kukagua ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga, pamoja na kuwasha umeme wa REA katika Kitongoji cha Mwanubi, Kolandoto.









