Moroco yaitoa kimasomaso Afrika

Morocco imekua timu pekee kutoka bara la Afrika kutinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia baada ya kuwatoa Spain kwa mikwaju ya Penati 3-0.

Spain ni kama hawakujiandaa kufika katika hatua ya penati kwani penati zao zote walizopiga walikosa.

Morocco wametangulia robo fainali kuwangoja kati ya Ureno au Uswizi ambao wanakutana kutafuta wa kuingia nae Morocco robo fainali.