Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko ya vituo kwa Mabalozi wawili na uteuzi wa Balozi mmoja kama ifuatavyo:

Amempangia Balozi Humphrey Herson Polepole kuiwakilisha Tanzania nchini Cuba. Kabla ya uteuzi huu Balozi Polepole alikuwa Balozi wa Tanzania, nchini Malawi.

Amemteua Balozi Lt. Jenerali (mstaafu) Yacoub Mohamed kuiwakilisha Tanzania katika Falme za Kiarabu (UAE). Kabla ya uteuzi huu, Balozi Mohamed alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Uturuki.

Amemteua Bw. Iddi Seif Bakari kuwa Balozi na kumpangia Ubalozi nchini Uturuki. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Bakari alikuwa Konseli Mkuu nchini Dubai.

Tarehe ya uapisho wa Balozi Bakari itatangazwa baadae.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

By Jamhuri