RAIS MAGUFULI AFUNGUA KITUO CHA MAFUNZO MAALUM YA KIJESHI MAPINGA MKOANI PWANI

  Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe kuashiria ufunguzi wa Kituo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi kilichopo Mapinga, Bagamoyo Mkoani Pwani. Wa Pili kushoto anayevuta utepe ni Naibu Mkuu wa Idara ya Usimamizi wa Mafunzo kutoka tume Kuu ya Kijeshi ya China Meja Jenerali Yang Jian na wa kwanza kushoto anayepiga makofi ni Balozi wa China hapa nchini Wang Ke.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania (CDF) Jenerali Venance Mabeyo mara baada ya kufungua Kituo hicho cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi kilichopo Mapinga, Bagamoyo Mkoani Pwani.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Naibu Mkuu wa Idara ya Usimamizi wa Mafunzo kutoka tume Kuu ya Kijeshi ya China Meja Jenerali Yang Jian mara baada ya ufunguzi wa kituo hicho ambacho kimejengwa kwa msaada kutoka Jeshi la Ukombozi la watu wa China.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt. Husein Mwinyi wakati alipokuwa akiandika jambo katika hotuba yake.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi mara baada ya kufungua Kituo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi kilichopo Mapinga, Bagamoyo Mkoani Pwani.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa China hapa nchini, Wang Ke mara baada ya kukifungua kituo hicho cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu Mkuu wa Idara ya Usimamizi wa Mafunzo kutoka tume Kuu ya Kijeshi ya China Meja Jenerali Yang Jian mara baada ya kukifungua kituo hicho cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo wakati alipokuwa akizungumza na Mbunge wa Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa, Mbunge wa Chalinze Ridhiwan Kikwete pamoja na Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo mara baada ya kufungua kituo hicho cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi.
 
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mapinga(hawaonekani pichani) waliokuwa wakiwasilisha kero mbalimbali za ardhi wakati alipokuwa akirejea jijini jijini Dar es Salaam mara baada ya kufungua kituo hicho cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi kilichopo Mapinga mkoani Pwani.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makomandoo wa JWTZ ambao walishiriki katika mazoezi ya Kijeshi kabla ya ufunguzi wa kituo hicho.
 Kikundi cha Ngoma za asili cha Makao makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikitumbuiza wakati wa sherehe za ufunguzi wa kituo hicho cha Mafunzo maalum ya Kijeshi kilichopo Mapinga mkoani Pwani.