Na John Mapepele – WAF, Washington, D.C.

Serikali ya Tanzania imekubaliana na Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C na Serikali ya Marekani kufanya utekelezaji wa kimkakati wa mkataba wa sekta ya afya ulioingiwa hivi karibuni ili kuzinufaisha pande zote mbili,huku wakiifanya Tanzania kuwa muhimili wa uzalishaji na usambazaji dawa na vifaa tiba Afrika.

Akizungumza katika Mkutano wa Wadau wa Ushirikiano wa Afya kati ya Marekani na Tanzania uliofanyika leo kati ya Serikali ya Tanzania na  Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C., na baadaye kufanya kikao  viongozi waandamizi Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Waziri wa Afya wa Tanzania, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa, alifafanua kuwa tayari Tanzania imejipanga vema kuhakikisha mkataba unatekelezwa kikamilifu.

Amesema Tanzania iko tayari kushirikiana na wawekezaji makini kutoka Marekani  na ipo tayari kupokea mtaji, teknolojia.

Akizungumzia historia ya muda mrefu baina ya nchi hizo, mhe Mchengerwa amefafanua kuwa 

Mwaka 1970, Rais wa wakati huo, Julius Nyerere, alishirikisha kampuni ya ushauri wa usimamizi kutoka Marekani, McKinsey & Company, kusaidia Tanzania kuimarisha mifumo ya uendeshaji wa serikali.

Amesema kazi hiyo ilichangia mageuzi ya ugatuzi wa madaraka ya mwaka 1972, ambayo yalisogeza huduma za serikali karibu zaidi na wananchi na kuanzisha muundo wa utawala wa mikoa na wilaya ambao unaendelea kuwa na ushawishi katika sekta ya umma ya Tanzania hadi leo.

Kwa Mchengerwa, umuhimu wa uzoefu huo hauishii kwenye historia. “McKinsey haikuiuza Tanzania bidhaa tu Iliisaidia nchi kujenga taasisi—taasisi ambayo ushawishi wake uliendelea kuwepo muda mrefu baada ya mkataba wa kampuni hiyo ya ushauri kumalizika”amesisitiza Mhe. Mchengerwa 

Alieleza kuwa huo ndio mtazamo ambao Tanzania inautafuta kutoka kwa wafanyabiashara wa Marekani leo: si miamala pekee, bali ushirikiano wenye uwezo wa kujenga taasisi, viwanda na uwezo unaodumu kwa vizazi ambapo Chama  cha Wafanyabiashara  wa Marekani  kimeahidi kuwaleta wawekezaji  wa madawa  nchini Tanzania ili kuja  kuona na  kuanza mashirikiano kwenye ene hili.

“Naomba  niwahakikishie  kuwa  Serikali ya Tanzania tayari imeshaweka mazingira rafik ya uwekezaji kwenye eneo la afya  na  hive ninavyoongea hapa  tayari kampını za  marekani  zimeanza  kufanya kazi” amesisitiza  Mhe. Mchengerwa.

Mhe. Mchengerwa ambaye ameambatana katika msafara wake na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia eneo la dawa na vifaa tiba, Emmanuel Tayari na Watendaji wakuu wa taasisi chini ya Wizara ya Afya alifafanua hatua kubwa iliyofikiwa katika sekta ya afya nchini.

Amesema  Chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, Tanzania imeanza kutekeleza mpango kabambe wa mageuzi ya kitaifa unaojengwa juu ya kile anachokiita katika 4R: Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Ujenzi Upya.