Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Jenista Mhagama akiongoza zoezi ufunguaji wa barabara na uondoaji wa tope katika Mji wa katesh Halmashauri ya Hanang’

Wananchi wamepokea kwa muitikio chanya zoezi la kuhifadhi waathirika wa maporomoko ya mawe na matope kutoka mlima Hanang kwa kushrikiana na Serikali. Uratibu wa zoezi hilo unaenda sanjari na ugawaji wa vifaa vya msaada wa kibinadamu kwa waathirika wa maafa hayo.

Hatua hiyo inaenda sambamba na hali ya urejeshaji hali katika mji wa Katesh, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang mkoani Manyara, huku shughuli ya uondoaji wa tope katika barabara na mitaa ya Mji wa Katesh ikiendelea.

By Jamhuri