Katika kutekeleza azimio la Viongozi wa nchi za Afrika, kupitia Mkutano wa Utoshelevu na Ustahimilivu wa Chakula (Dakar 2 Summit on Feed Africa: Food Sovereignty and Resilience) uliofanyika Dakar, Senegal Januari 25 hadi 27 , 2023, waliazimia kila nchi kuunda Mabaraza ya kusimamia utekelezaji wa mikakati ya kukuza kilimo na kuongeza uzalishaji wa chakula (Presidential Food and Agriculture Delivery Council). Ili kufikia azma hiyo;

Rais Samia Suluhu Hassan ameunda Baraza la Kumshauri Rais kuhusu Utekelezaji wa Masuala ya Kilimo na Chakula (Presidential Food and Agriculture Delivery Council); na amemteua Mizengo Kayanza Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo.

Aidha,Rais amewateua Geoffrey Kirenga, Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT na Andrew Masawe, Katibu Mkuu Mstaafu kuwa Wajumbe wa Baraza hilo.

Vilevile Rais, amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Sekretarieti ya Baraza:Dkt. Florence Turuka, Katibu Mkuu Mstaafu na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA); Dkt. Jacqueline Mkindi, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Horticulture Association (TAHA); na

Dkt. Mwatima Juma, Mwenyekiti wa Tanzania Organic Agricultural Movement (TOAM).Baraza hilo litazinduliwa tarehe 17 Machi, 2023 Ikulu, Dar es Salaam.

By Jamhuri