AGIZO LA WAZIRI MKUU KWA MAWAZIRI WANAISHI DAR ES SALAAM

Disemba 12 mwaka huu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliandika barua kwenda kwa Mawaziri, Manaibu Waziri, Wakurugenzi na watumishi wengine wa serikali ambao hawakai kwenye vituo vyao vya kazi kwa mujibu wa sheria, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa agizo hilo kufuatia kuwapo kwa mawaziri na viongozi wengine ambao wamepangiwa kuhamia Dodoma, kuendelea kukaa Dar es Salaam, badala ya vituo vyao.