Ndege ndogo imeanguka kwenye uwanja wa ndege karibu na mji mkuu wa Poland Warsaw, na kuua watu watano akiwemo rubani wake, maafisa wanasema.

Watu wanane pia walijeruhiwa katika ajali hiyo, polisi wanasema.

Watu kumi na watatu walikuwa wameripotiwa kujikinga kwenye banda la ndege kutokana na hali mbaya ya hewa.

Kikosi cha zima moto kilisema hali mbaya ya hewa ilikuwa “sababu inayowezekana” ya ajali hiyo.

Helikopta nne na ambulensi 10 zilitumwa kwenye eneo la tukio katika kijiji cha Chrcynno.

Kijiji kiko 47km (maili 29) kutoka mji mkuu Warsaw.

Vyombo vya habari vya Poland viliitambua ndege iliyoanguka kama Cessna 208.

Idara ya zima moto ya eneo hilo ilithibitisha kisa hicho kilichotokea katika uwanja wa ndege huko Chrcynno na kuweka picha kwenye Facebook ikionyesha mkia wa ndege hiyo ukitoka kwenye banda la ndege.

Polisi waliarifiwa muda mfupi baada ya 17:30 GMT, shirika la habari la AFP linaripoti.

Waokoaji wanasema watu watatu walikuwa ndani ya ndege hiyo ilipogongana na bati kwenye eneo la banda la ndege, shirika la habari la AFP linaongeza.

By Jamhuri