Cameroon imethibitisha kufanya mazungumzo na kocha wa zamani wa England Sven-Goran Eriksson kuchukua usukani wa kuifunza timu ya taifa hilo Indomitable Lions.

Eriksson mwenye umri wa miaka , 70, raia wa Sweden alikuwa na mazungumzo mazuri na maafisa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Cameroon (Fecafoot) mjini Yaoundé wiki iliyopita waliokuwa wakitaka kuziba pengo lililoachwa baada ya kuondoka kwa Hugo Broos.

“Baada ya kukaa saa 72, Sven-Goran Eriksson aliondoka Yaoundé Jumamosi tarehe 28 July 2018,” Fecafool lilieleza kwenye ukurasa wake wa Twitter.

” Meneja huyo raia wa Sweden alikuwa amekaribishwa na Cameroon kwa mazungumzo juu ya kuajiriwa kwa kocha mkuu wa timu kuu ya taifa – the Indomitable Lions.

” Baada ya kumpa mtihani wa kazi Sven-Goran Eriksson na kuzingatia mapendekezo mengine yaliyopo, Fecafoot litafichua chaguo lake la kocha wa kudumu wa timu yetu ya taifa lilieleza shirikisho hilo la mpira wa miguu la Cameroon.

Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Aliyekuwa kocha wa timu ya Indomitable Lions Hugo Broos, aliondoka mwezi Februari mwaka huu baada ya mkataba wake kuisha

Eriksson, ambae alikuwa meneja wa England kati ya mwaka 2001 na 2006, na kuifikisha timu hiyo hadi michuano ya robo fainali ya Kombe la Dunia mara mbili, alikuwa mmoja wa watu 77 ambao maombi yao ya kazi yalifichuliwa mwezi Aprili.

BBC inafahamu kuwa Eriksson, ambaye awali alikuwa mkufunzi wa klabu za England Manchester City na Leicester City, atalipwa CFA 50 million (€71,000) kila mwezi na atafanya kazi na kocha msaidizi raia wa Cameroon na ataishi nchini humo.

Vyombo vya habari nchini Cameroon pia vimewahusisha Waholanzi Clarence Seedorf na Patrick Kluivert na kazi hiyo. 

Awali Eriksson alizifunza timu za Mexico na akafanikiwa kuipeleka led Ivory Coast katika Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini kabla ya kuwa meneja wa timu ya Uchina ya Guangzhou Evergrande mnamo 2013.

Akiwa Uchina pia alipata fursa ya kuzifunza timu za Shanghai SIPG na Shenzhen, kabla ya kuondoka hukomwezi June 2017.

Pia amekuwa akihusishwa na Iraq kama kocha.

Kazi ya kocha wa timu ya Cameroon ilikuwa wazi mwezi Februari wakati aliekuwa kocha wa timu Indomitable Lions Hugo Broos, alipoondoka baada ya mkataba wake kuisha.

By Jamhuri